06-Matendo Mema Na Athari Yake Katika Utajiri Na Ukunjufu Wa Rizki: Faida Ya Rizki Ya Halali Katika Dunia Na Akhera

 

E. FAIDA YA RIZKI YA HALALI DUNIANI NA AKHERA

 

1. FAIDA KATIKA DUNIA

 

(A) KUJIBIWA DUA

 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema nilisoma hii aya mbele ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam): “Enyi watu kuleni vilivyomo ardhini vilivyo halali vizuri.” akasimama Sa’ad bin Abi waqaas akasema: ewe Mtume wa Allaah niombee Allaah Anijaalie du’aa zangu zijibiwe, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam) akamwambia, “Ewe Sa’ad! Kula cha halali utakuwa mwenye kujibiwa du’aa, naapa kwa yule nafsi ya Muhammad ipo mkononi mwake hakika mja ananyakua tonge la haramu kuingiza mdomoni mwake haikubaliwi matendo yake siku arobaini na mja yoyote nyama yake inaota kwa haramu basi moto ni bora kwake.”

 

 

(B) BARAKA KATIKA MALI MKE NA WATOTO

 

(C) RAHA KATIKA NAFSI

 

Anayechunga kula halali anasalimika na midomo ya watu, watakuwa wanamtaja kwa uzuri na watakuwa naye mahusiano mazuri.

 

 

FAIDA KATIKA AKHERA

 

1. KUINGIA PEPONI

 

Kutoka kwa Abu Sa’iid Al-Khudriy amesema, amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

Mwenye kula halali na akatenda katika mwenendo wa Mtume na watu wakasalimika na shari yake ataingia peponi.” At-Tirmidhiy.

 

Wakasema ewe Mtume wa Allaah hilo katika umati wako leo ni wengi. Akasema na itakuwa katika karne baada yangu.

 

 

2. KUSAMEHEWA MADHAMBI

 

 Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

 

“Mwenye kulala hali ya kula cha halali alichokichuma analala hali ya kuwa amesamehewa.”

 

 

3. ATAPATA UNAFUU SIKU YA QIYAAMAH (HESABU)

 

4. KUKUBALIWA SADAKA YAKE NA KULIPWA MARADUFU

 

Kutoka kwa Abu Hurayrah amesema, amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

 

“Mwenye kutoa sadaka usawa wa tende katika chumo la halali na Allaah Hapokei ila vilivyo vizuri, na Allaah Anapokea kwa mkono wa kulia kisha Anamlelea mtoaji, kama mmoja wenu anavyomlea mtoto wa ngamia, mpaka iwe mfano wa jabali.” Al-Bukhaariy

 

 

5. KUJIEPUSHA NA HARAMU

 

Amekataza Allaah chumo la haramu Aliposema,

 

“Enyi mlioamini msiliane mali zenu kwa batili. isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana baina yenu. (hiyo inajuzu) wala msijiue wala msiue (wenzenu). Hakika Allaah ni mwenye kukuhurumieni.

Na atakayefanya haya kwa uadui na dhulma, basi huyo tutamuingiza motoni. Na hayo ni rahisi kwa Allaah.) An-Nisaa: 29-30

 

Anasema Allaah:

 

(Allaah Amehalalisha biashara na Akaiharamisha riba.” Al-Baqarah: 275

 

Amesema Ibn ‘Abbaas: “Ataambiwa mla riba siku ya Qiyaamah chukua silaha yako kwa vita na Allaah.”

 

Share