Kulipa Pesa Kila Mwezi Kwa Ajili Ya Bima Ya Uzima Inafaa?

SWALI:

 

Assalam aleikum. Nipo namasuali! Sheria ya kiislam yamruhusu mtu kujiunga na NHiF kulipa pesa kila mwezi kwa kujiekea utakapokua mgonjwa watakulipia hospital!!


 

 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Kwanza kabisa tunapenda kuwakumbusha wote wenye kuzoea kufupisha Salaam au kufupisha kumswalia Mtume wetu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) au kufupisha kumtukuza Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), ni bora waache kufanya hivyo na waandike kwa urefu kwani zote hizo ni 'Ibaadah na ni bora kuzifanya kwa ukamilifu ikiwemo katika kuandika, kutamka n.k. Pia kuongeza neno 'Ta'ala' kwenye Salaam kwa kusema 'Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaahi Ta'ala wa Barakaatuh', si jambo tulilofundishwa katika Salaam na hivyo ni bora mtu kuliepuka katika Salaam.

 

 

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kulipa pesa kila mwezi kwa ajili ya bima ya afya na siha.

Hakika ni kuwa suala la bima tumelizungumzia kwa kina katika maswali kadhaa yalikuja kwetu kwa ufumbuzi.

 

Suala hilo halifai katika shari’ah yetu kwa kuwa lina vipengele vifuatavyo:

 

1.      Kuna kamari ndani yake.

2.      Udanganyifu.

3.      Kulipa bila kupata huduma kwa malipo yako.

 

Kwa ajili hiyo, bima ya uzima haifai kisheria. Hata hivyo, ikiwa unaishi katika nchi ambayo imelazimishwa kama kipengele muhimu kwa mfanyakazi, kwa hali hiyo wewe utaendelea kufanya kazi hapo na utakuwa unalipa au kukatwa katika mshahara wako na huku unachukia, lakini kwa kulipa na huku unaridhia japokuwa si sharti katika nchi unayoishi itakuwa haifai.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share