Kufanya Hajj Na Huku Familia Yake Inalishwa Na Serikali Ulaya; Hawakusema Serikalini Kuwa Wameoana

 

Kufanya Hajj Na Huku Familia Yake Inalishwa Na Serikali Ulaya; Hawakusema Serikalini Kuwa Wameoana

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali:

 

Assalam Alaykum Warahmatullah

 

Mimi Naomba Niulizie Kuhusu Mtu Ambae Anataka Kwenda Kutekeleza Ibada Ya Hajj Na Anouwezo Wa Kiafya Na Kifedha Za Kuachia Mke Wake Na Watoto Wake Kwa Ajili Ya Matumizi Yao, Lakini Nyumba Wanayokaa Wanalipiwa Na Serikali Kwa Sababu Hawakusema Kwamba Wameoana Jee Inafaa Au Akiilipia Kwa Muda Mfupi Tu Ili Katika Kile Kipindi Cha Kua Yeye Yuko Katika Ibada Hio Ya Hajj Awe Amejilipia Mwenyewe Jee Inafaa?

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Kuiambia serikali kuwa hajaona na mkewe au kuiambia kuwa wametengena na mkewe na hali hawajatengana; hayo ni makosa na ni mambo ambayo yanaweza hata kumtenganisha mtu na mkewe kutegemea na makusudio yake.

 

Hivyo, atakuwa amefanya makosa kwa udanganyifu wake ambao umesababishwa na maslahi madogo tu ya kidunia ya kubana pesa za kulipia nyumba kwa ajili ya kujilimbikizia mali ili ima ajenge kwao alipotoka au aanzishe biashara n.k.

 

Mtu huyo atakuwa na madhambi mbele ya Allaah Aliyetukuka kwa kuongopa kwake. Hakika huko ni kuudhalilisha Uislamu wake kwa Makafiri na hata kumtukunisha mkewe ambaye pindi atakapoonekama amebeba mimba italeta picha ya kuwa Muislamu huyo ni malaya.

 

Tafadhali soma zaidi yaliyomo kwenye viungo vifuatavyo:

 

Nasaha Kwa Wakimbizi Wanaoishi Kusema Hawajaoana Ili Wapate Ruzuku Ya Serikali

 

Anapewa Pesa Na Serikali, Je, Mume Hapasi Kumhudumia Ikiwa Ni Hivyo?

 

Hata hivyo, ‘Ibaadah yake ya Hijjah ikiwa chumo lake ni la halali itakuwa ni sawa na itabidi aombe msamaha kwa Allaah Aliyetukuka na atoke katika nyumba ambayo ameipata kwa udanganyifu.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share