025 - Al-Furqaan

 

  الْفُرْقان

 

 

025-Al-Furqaan

 

024-Al-Furqaan: Utangulizi Wa Suwrah

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

 

 

تَبَارَكَ الَّذِي نَزَّلَ الْفُرْقَانَ عَلَىٰ عَبْدِهِ لِيَكُونَ لِلْعَالَمِينَ نَذِيرًا ﴿١﴾

1. Amebarikika Ambaye Ameteremsha kwa Mja Wake pambanuo[1] ili awe muonyaji kwa walimwengu.

 

 

 

الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَلَمْ يَتَّخِذْ وَلَدًا وَلَمْ يَكُن لَّهُ شَرِيكٌ فِي الْمُلْكِ وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا ﴿٢﴾

2. Ambaye Ni Wake Pekee ufalme wa mbingu na ardhi, na Hakujichukulia mwana wala Hakuwa na mshirika katika ufalme, na Ameumba kila kitu, kisha Akakikadiria kipimo cha sawa sawa.

 

 

 

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِهِ آلِهَةً لَّا يَخْلُقُونَ شَيْئًا وَهُمْ يُخْلَقُونَ وَلَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا وَلَا يَمْلِكُونَ مَوْتًا وَلَا حَيَاةً وَلَا نُشُورًا ﴿٣﴾

3. Na wakachukua badala Yake (Allaah) waabudiwa wasioumba chochote na hali wao wanaumbwa, wala hawamiliki kwa ajili ya nafsi zao dhara wala manufaa, wala hawamiliki mauti wala uhai wala ufufuo.

 

 

 

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا إِفْكٌ افْتَرَاهُ وَأَعَانَهُ عَلَيْهِ قَوْمٌ آخَرُونَ ۖ فَقَدْ جَاءُوا ظُلْمًا وَزُورًا ﴿٤﴾

4. Wakasema wale waliokufuru: Hii (Qur-aan) si chochote isipokuwa ni uzushi alioutunga (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), na wamemsaidia watu wengine. Kwa yakini wameleta dhulma na uongo.[2]

 

 

 

وَقَالُوا أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ اكْتَتَبَهَا فَهِيَ تُمْلَىٰ عَلَيْهِ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٥﴾

5. Na wakasema: Ni hekaya za kale ameziandikisha kisha anasomewa asubuhi na jioni.

 

 

 

قُلْ أَنزَلَهُ الَّذِي يَعْلَمُ السِّرَّ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ إِنَّهُ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٦﴾

6. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Ameiteremsha Ambaye Anajua siri katika mbingu na ardhi. Hakika Yeye daima Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu. 

 

 

 

وَقَالُوا مَالِ هَـٰذَا الرَّسُولِ يَأْكُلُ الطَّعَامَ وَيَمْشِي فِي الْأَسْوَاقِ ۙ لَوْلَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مَلَكٌ فَيَكُونَ مَعَهُ نَذِيرًا ﴿٧﴾

7. Na wakasema: Ni Rasuli gani huyu? Anakula chakula na anatembea masokoni! Kwa nini asiteremshiwe Malaika akawa muonyaji pamoja naye?[3]

 

 

 

أَوْ يُلْقَىٰ إِلَيْهِ كَنزٌ أَوْ تَكُونُ لَهُ جَنَّةٌ يَأْكُلُ مِنْهَا ۚ وَقَالَ الظَّالِمُونَ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلًا مَّسْحُورًا ﴿٨﴾

8. Au aangushiwe hazina juu yake au awe na bustani awe anakula humo? Na wakasema madhalimu: Hamfuati isipokuwa mtu aliyerogwa.

 

 

 

انظُرْ كَيْفَ ضَرَبُوا لَكَ الْأَمْثَالَ فَضَلُّوا فَلَا يَسْتَطِيعُونَ سَبِيلًا ﴿٩﴾

9. Tazama vipi walivyokupigia mifano, basi wamepotea, hawatoweza kupata njia (ya haki).

 

 

 

تَبَارَكَ الَّذِي إِن شَاءَ جَعَلَ لَكَ خَيْرًا مِّن ذَٰلِكَ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَيَجْعَل لَّكَ قُصُورًا ﴿١٠﴾

10. Amebarikika Ambaye Akitaka Atakujaalia kheri kuliko hayo; ni Jannaat zipitazo katikati yake mito na Akujaalie maqasri.

 

 

 

بَلْ كَذَّبُوا بِالسَّاعَةِ ۖ وَأَعْتَدْنَا لِمَن كَذَّبَ بِالسَّاعَةِ سَعِيرًا ﴿١١﴾

11. Bali wameikadhibisha Saa. Na Tumeandaa kwa anayeikadhibisha Saa moto uliowashwa vikali mno. 

 

 

 

إِذَا رَأَتْهُم مِّن مَّكَانٍ بَعِيدٍ سَمِعُوا لَهَا تَغَيُّظًا وَزَفِيرًا ﴿١٢﴾

12. (Moto huo) Utakapowaona kutoka mahali mbali, watausikia ghadhabu zake na mngurumo wake.

 

 

 

وَإِذَا أُلْقُوا مِنْهَا مَكَانًا ضَيِّقًا مُّقَرَّنِينَ دَعَوْا هُنَالِكَ ثُبُورًا ﴿١٣﴾

13. Na watakapotupwa humo mahali pa dhiki wakiwa wamefungashwa pamoja wataomba huko kuteketea. 

 

 

 

لَّا تَدْعُوا الْيَوْمَ ثُبُورًا وَاحِدًا وَادْعُوا ثُبُورًا كَثِيرًا ﴿١٤﴾

14. Msiombe leo kuteketea kumoja, bali ombeni kuteketea kwingi!

 

 

 

قُلْ أَذَٰلِكَ خَيْرٌ أَمْ جَنَّةُ الْخُلْدِ الَّتِي وُعِدَ الْمُتَّقُونَ ۚ كَانَتْ لَهُمْ جَزَاءً وَمَصِيرًا ﴿١٥﴾

15. Sema: Je, hayo ni bora, au Jannah ya yenye kudumu ambayo wameahidiwa wenye taqwa? Itakuwa kwao ni jazaa na mahali pa kuishia.

 

 

 

لَّهُمْ فِيهَا مَا يَشَاءُونَ خَالِدِينَ ۚ كَانَ عَلَىٰ رَبِّكَ وَعْدًا مَّسْئُولًا ﴿١٦﴾

16. Watapata humo kila wanachokitaka, wadumu milele. Imekuwa ni ahadi juu ya Rabb wako ya kuombwa.

 

 

 

وَيَوْمَ يَحْشُرُهُمْ وَمَا يَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ فَيَقُولُ أَأَنتُمْ أَضْلَلْتُمْ عِبَادِي هَـٰؤُلَاءِ أَمْ هُمْ ضَلُّوا السَّبِيلَ ﴿١٧﴾

17. Na Siku Atakayowakusanya pamoja na yale wanayoyaabudu badala ya Allaah Aseme: Je, ni nyinyi ndio mliowapoteza Waja Wangu, au wao ndio waliopotea njia?

 

 

 

قَالُوا سُبْحَانَكَ مَا كَانَ يَنبَغِي لَنَا أَن نَّتَّخِذَ مِن دُونِكَ مِنْ أَوْلِيَاءَ وَلَـٰكِن مَّتَّعْتَهُمْ وَآبَاءَهُمْ حَتَّىٰ نَسُوا الذِّكْرَ وَكَانُوا قَوْمًا بُورًا ﴿١٨﴾

18. Watasema: Subhaanak! (Utakasifu ni Wako!) Haikutupasa sisi kuchukua badala Yako rafiki walinzi wowote, lakini Uliwastarehesha na baba zao mpaka wakasahau ukumbusho na wakawa watu wa kuteketea.

 

 

 

فَقَدْ كَذَّبُوكُم بِمَا تَقُولُونَ فَمَا تَسْتَطِيعُونَ صَرْفًا وَلَا نَصْرًا ۚ وَمَن يَظْلِم مِّنكُمْ نُذِقْهُ عَذَابًا كَبِيرًا ﴿١٩﴾

19. Basi wamekwisha kukadhibisheni kwa yale myasemayo, hivyo hamtoweza kujiondoshea wala kujinusuru. Na yeyote atakayedhulumu miongoni mwenu Tutamuonjesha adhabu kubwa.

 

 

 

وَمَا أَرْسَلْنَا قَبْلَكَ مِنَ الْمُرْسَلِينَ إِلَّا إِنَّهُمْ لَيَأْكُلُونَ الطَّعَامَ وَيَمْشُونَ فِي الْأَسْوَاقِ ۗ وَجَعَلْنَا بَعْضَكُمْ لِبَعْضٍ فِتْنَةً أَتَصْبِرُونَ ۗ وَكَانَ رَبُّكَ بَصِيرًا ﴿٢٠﴾

20. Na Hatukupeleka kabla yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Rusuli wowote isipokuwa bila shaka wakila chakula, na wanatembea masokoni. Na Tumejaalia baadhi yenu nyinyi kwa nyinyi kuwa ni majaribio.[4] Je, mtasubiri? Na Rabb wako Ni Mwenye Kuona daima.

 

 

 

وَقَالَ الَّذِينَ لَا يَرْجُونَ لِقَاءَنَا لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْنَا الْمَلَائِكَةُ أَوْ نَرَىٰ رَبَّنَا ۗ لَقَدِ اسْتَكْبَرُوا فِي أَنفُسِهِمْ وَعَتَوْا عُتُوًّا كَبِيرًا ﴿٢١﴾

21. Na walisema wale wasiotaraji kukutana Nasi: Kwa nini hatuteremshiwi Malaika, au hatumwoni Rabb wetu? Kwa yakini wametakabari katika nafsi zao na wakavuka mipaka ya ufedhuli na uasi mkubwa.[5]

 

 

 

يَوْمَ يَرَوْنَ الْمَلَائِكَةَ لَا بُشْرَىٰ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُجْرِمِينَ وَيَقُولُونَ حِجْرًا مَّحْجُورًا ﴿٢٢﴾

22. Siku watakayowaona Malaika hakutakuwa na bishara njema Siku hiyo kwa wakhalifu na (Malaika) watasema: Marufuku tena marufuku kabisa (nyinyi kupata mafanikio yoyote leo).[6]

 

 

 

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

23. Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zikitawanyika.[7]

 

 

 

أَصْحَابُ الْجَنَّةِ يَوْمَئِذٍ خَيْرٌ مُّسْتَقَرًّا وَأَحْسَنُ مَقِيلًا ﴿٢٤﴾

24. Watu wa Jannah Siku hiyo watakuwa katika makazi bora ya kustakiri, na mahali pazuri kabisa pa kupumzikia.

 

 

 

وَيَوْمَ تَشَقَّقُ السَّمَاءُ بِالْغَمَامِ وَنُزِّلَ الْمَلَائِكَةُ تَنزِيلًا ﴿٢٥﴾

25. Na Siku itakayofunguka mbingu kwa mawingu, na Malaika watateremshwa mteremsho mkubwa wa mfuatano.[8]

 

 

 

الْمُلْكُ يَوْمَئِذٍ الْحَقُّ لِلرَّحْمَـٰنِ ۚ وَكَانَ يَوْمًا عَلَى الْكَافِرِينَ عَسِيرًا ﴿٢٦﴾

26. Ufalme wa haki Siku hiyo utakuwa ni wa Ar-Rahmaan. Na itakuwa ni siku ngumu kwa makafiri.

 

 

 

وَيَوْمَ يَعَضُّ الظَّالِمُ عَلَىٰ يَدَيْهِ يَقُولُ يَا لَيْتَنِي اتَّخَذْتُ مَعَ الرَّسُولِ سَبِيلًا ﴿٢٧﴾

27. Na siku dhalimu atakapouma mikono yake akisema: Laiti ningeshika njia pamoja na Rasuli.[9] 

 

 

 

يَا وَيْلَتَىٰ لَيْتَنِي لَمْ أَتَّخِذْ فُلَانًا خَلِيلًا ﴿٢٨﴾

28. Ee ole wangu! Laiti nisingelimfanya fulani kuwa rafiki mwandani.

 

 

 

لَّقَدْ أَضَلَّنِي عَنِ الذِّكْرِ بَعْدَ إِذْ جَاءَنِي ۗ وَكَانَ الشَّيْطَانُ لِلْإِنسَانِ خَذُولًا ﴿٢٩﴾

29. Kwa yakini amenipoteza mbali na Ukumbusho baada ya kunijia. Na shaytwaan kwa binaadam daima ni msaliti.

 

 

 

وَقَالَ الرَّسُولُ يَا رَبِّ إِنَّ قَوْمِي اتَّخَذُوا هَـٰذَا الْقُرْآنَ مَهْجُورًا ﴿٣٠﴾

30. Na Rasuli akasema: Rabb wangu! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur-aan yenye kuhamwa.[10]

 

 

 

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوًّا مِّنَ الْمُجْرِمِينَ ۗ وَكَفَىٰ بِرَبِّكَ هَادِيًا وَنَصِيرًا ﴿٣١﴾

31. Na hivyo ndivyo Tumemfanyia kila Nabiy adui miongoni mwa wakhalifu. Na Rabb wako Anatosheleza kuwa ni Mwenye Kuongoza na Mwenye Kunusuru.

 

 

 

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْلَا نُزِّلَ عَلَيْهِ الْقُرْآنُ جُمْلَةً وَاحِدَةً ۚ كَذَٰلِكَ لِنُثَبِّتَ بِهِ فُؤَادَكَ ۖ وَرَتَّلْنَاهُ تَرْتِيلًا ﴿٣٢﴾

32. Na wakasema wale waliokufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur-aan kwa ujumla mara moja tu? Ndio hivyo hivyo, ili Tukithibitishe kifua chako. Na Tumeifunulia Wahyi punde kwa punde kwa kuratibu. [11]

 

 

 

وَلَا يَأْتُونَكَ بِمَثَلٍ إِلَّا جِئْنَاكَ بِالْحَقِّ وَأَحْسَنَ تَفْسِيرًا ﴿٣٣﴾

33. Na wala hawakujii kwa mfano wowote isipokuwa Tunakuletea haki na tafsiri nzuri kabisa.

 

 

 

الَّذِينَ يُحْشَرُونَ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ إِلَىٰ جَهَنَّمَ أُولَـٰئِكَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضَلُّ سَبِيلًا ﴿٣٤﴾

34. Wale ambao watakusanywa juu ya nyuso zaokuelekea Jahannam[12], hao wana mahali pabaya mno, na wamepotea zaidi njia.

 

 

 

وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ وَجَعَلْنَا مَعَهُ أَخَاهُ هَارُونَ وَزِيرًا ﴿٣٥﴾

35. Na kwa yakini Tulimpa Muwsaa Maandiko (ya Tawraat) na Tukamjaalia pamoja naye kaka yake Haaruwn kuwa msaidizi.

 

 

 

فَقُلْنَا اذْهَبَا إِلَى الْقَوْمِ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا فَدَمَّرْنَاهُمْ تَدْمِيرًا ﴿٣٦﴾

36. Tukasema: Nendeni kwa watu ambao wamekadhibisha Aayaat (Ishara, Dalili) Zetu, basi Tukawadamirisha vibaya.  

 

 

 

وَقَوْمَ نُوحٍ لَّمَّا كَذَّبُوا الرُّسُلَ أَغْرَقْنَاهُمْ وَجَعَلْنَاهُمْ لِلنَّاسِ آيَةً ۖ وَأَعْتَدْنَا لِلظَّالِمِينَ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿٣٧﴾

37. Na watu wa Nuwh walipowakadhibisha Rusuli, Tuliwagharikisha, na Tukawafanya kuwa Aayah (Mazingatio) kwa watu. Na Tumewaandalia madhalimu adhabu iumizayo.

 

 

 

وَعَادًا وَثَمُودَ وَأَصْحَابَ الرَّسِّ وَقُرُونًا بَيْنَ ذَٰلِكَ كَثِيرًا ﴿٣٨﴾

38. Na kina ‘Aad na Thamuwd na watu wa Ar-Rass[13] na karne nyingi zilizokuwa baina yao.

 

 

 

وَكُلًّا ضَرَبْنَا لَهُ الْأَمْثَالَ ۖ وَكُلًّا تَبَّرْنَا تَتْبِيرًا ﴿٣٩﴾

39. Na kila mmoja Tuliwapigia mifano na kila mmoja Tuliwateketeza mateketezo kamilifu.

 

 

 

وَلَقَدْ أَتَوْا عَلَى الْقَرْيَةِ الَّتِي أُمْطِرَتْ مَطَرَ السَّوْءِ ۚ أَفَلَمْ يَكُونُوا يَرَوْنَهَا ۚ بَلْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ نُشُورًا ﴿٤٠﴾

40. Na kwa yakini walipita katika mji ambao ulinyeshewa mvua mbaya. Je, basi hawakuwa wakiuona? Bali walikuwa hawataraji kufufuliwa.

 

 

 

وَإِذَا رَأَوْكَ إِن يَتَّخِذُونَكَ إِلَّا هُزُوًا أَهَـٰذَا الَّذِي بَعَثَ اللَّـهُ رَسُولًا ﴿٤١﴾

41. Na wanapokuona (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) hawakuchukulii isipokuwa mzaha (wakisema): Je, ndiye huyu ambaye Allaah Amemtuma kuwa Rasuli?

 

 

 

إِن كَادَ لَيُضِلُّنَا عَنْ آلِهَتِنَا لَوْلَا أَن صَبَرْنَا عَلَيْهَا ۚ وَسَوْفَ يَعْلَمُونَ حِينَ يَرَوْنَ الْعَذَابَ مَنْ أَضَلُّ سَبِيلًا ﴿٤٢﴾

42. Kwa yakini alikaribia kutupoteza na waabudiwa wetu, ingelikuwa hatukuvumilia kuwaabudu. Lakini watakuja kujua wakati watakapoona adhabu, ni nani aliyepotea zaidi njia.

 

 

 

أَرَأَيْتَ مَنِ اتَّخَذَ إِلَـٰهَهُ هَوَاهُ أَفَأَنتَ تَكُونُ عَلَيْهِ وَكِيلًا ﴿٤٣﴾

43. Je, umemuona yule aliyefanya hawaa yake kuwa ndio mwabudiwa wake?  Je, basi utaweza wewe kuwa ni mdhamini wake?[14]

 

 

 

أَمْ تَحْسَبُ أَنَّ أَكْثَرَهُمْ يَسْمَعُونَ أَوْ يَعْقِلُونَ ۚ إِنْ هُمْ إِلَّا كَالْأَنْعَامِ ۖ بَلْ هُمْ أَضَلُّ سَبِيلًا ﴿٤٤﴾

44. Je, unadhania kwamba wengi wao wanasikia au wanatia akilini? Wao si chochote isipokuwa kama wanyama, bali wao wamepotea zaidi njia.

 

 

 

أَلَمْ تَرَ إِلَىٰ رَبِّكَ كَيْفَ مَدَّ الظِّلَّ وَلَوْ شَاءَ لَجَعَلَهُ سَاكِنًا ثُمَّ جَعَلْنَا الشَّمْسَ عَلَيْهِ دَلِيلًا ﴿٤٥﴾

45. Je, huoni vipi Rabb wako Alivyotandaza kivuli? Angelitaka Angelikifanya kitulie tu kisha Tukalifanya jua kuwa kielekezo juu yake.

 

 

 

ثُمَّ قَبَضْنَاهُ إِلَيْنَا قَبْضًا يَسِيرًا ﴿٤٦﴾

46. Kisha Tunakivutia Kwetu mvuto wa polepole.

 

 

 

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ اللَّيْلَ لِبَاسًا وَالنَّوْمَ سُبَاتًا وَجَعَلَ النَّهَارَ نُشُورًا ﴿٤٧﴾

47. Naye Ndiye Ambaye Amekujaalieni usiku kuwa ni libasi na usingizi wa mapumziko ya kama kufa, na Amefanya mchana ni wa kuinuka na kutawanyika.

 

 

 

وَهُوَ الَّذِي أَرْسَلَ الرِّيَاحَ بُشْرًا بَيْنَ يَدَيْ رَحْمَتِهِ ۚ وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً طَهُورًا ﴿٤٨﴾

48. Naye Ndiye Ambaye Ametuma upepo wa kheri kuwa bishara njema kabla ya Rehma Yake. Na Tunateremsha kutoka mbinguni maji yaliyo safi.

 

 

 

لِّنُحْيِيَ بِهِ بَلْدَةً مَّيْتًا وَنُسْقِيَهُ مِمَّا خَلَقْنَا أَنْعَامًا وَأَنَاسِيَّ كَثِيرًا ﴿٤٩﴾

49. Ili Tuhuishe kwayo nchi iliyokufa,[15] na Tuwanyweshe kwayo kati ya wale Tuliowaumba; wanyama na watu wengi.

 

 

 

وَلَقَدْ صَرَّفْنَاهُ بَيْنَهُمْ لِيَذَّكَّرُوا فَأَبَىٰ أَكْثَرُ النَّاسِ إِلَّا كُفُورًا ﴿٥٠﴾

50. Na kwa yakini Tumeigawa (mvua) baina yao ili wakumbuke (Neema za Allaah), lakini watu wengi wanakataa kabisa, (hawana) isipokuwa kukufuru tu.

 

 

 

وَلَوْ شِئْنَا لَبَعَثْنَا فِي كُلِّ قَرْيَةٍ نَّذِيرًا ﴿٥١﴾

51. Na lau Tungelitaka, bila shaka Tungelipeleka katika kila mji mwonyaji.

 

 

 

فَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَجَاهِدْهُم بِهِ جِهَادًا كَبِيرًا ﴿٥٢﴾

52. Basi usiwatii makafiri. Na pambana nao kwayo (Qur-aan) kwa juhudi za upeo wako wa mwisho.

 

 

 

وَهُوَ الَّذِي مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ هَـٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ وَهَـٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ وَجَعَلَ بَيْنَهُمَا بَرْزَخًا وَحِجْرًا مَّحْجُورًا ﴿٥٣﴾

53. Naye Ndiye Aliyeunganisha bahari mbili; hii ni tamu ikatayo kiu, na hii ni ya chumvi, kali. Na Akajaalia baina yao kitenganisho na kizuizi kinachozuia kabisa.[16]

 

 

 

وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ مِنَ الْمَاءِ بَشَرًا فَجَعَلَهُ نَسَبًا وَصِهْرًا ۗ وَكَانَ رَبُّكَ قَدِيرًا ﴿٥٤﴾

54. Naye Ndiye Aliyeumba mtu kutokana na maji, kisha Akamjaalia kuwa na unasaba wa damu na uhusiano wa ndoa. Na Rabb wako daima Ni Mweza wa yote.

 

 

 

وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُهُمْ وَلَا يَضُرُّهُمْ ۗ وَكَانَ الْكَافِرُ عَلَىٰ رَبِّهِ ظَهِيرًا ﴿٥٥﴾

55. Na wanaabudu badala ya Allaah vile visivyowafaa na visivyowadhuru. Na kafiri daima ni msaidizi wa kumpinga Rabb wake.

 

 

 

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا مُبَشِّرًا وَنَذِيرًا ﴿٥٦﴾

56. Na Hatukukutuma (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) isipokuwa ni mbashiriaji na mwonyaji.

 

 

 

قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِلَّا مَن شَاءَ أَن يَتَّخِذَ إِلَىٰ رَبِّهِ سَبِيلًا ﴿٥٧﴾

57. Sema: Sikuombeni ujira juu yake isipokuwa atakaye achukue njia kuelekea kwa Rabb wake.

 

 

 

وَتَوَكَّلْ عَلَى الْحَيِّ الَّذِي لَا يَمُوتُ وَسَبِّحْ بِحَمْدِهِ ۚ وَكَفَىٰ بِهِ بِذُنُوبِ عِبَادِهِ خَبِيرًا ﴿٥٨﴾

58. Na tawakali kwa Aliye Hai Ambaye Hafi, na sabihi ukimhimidi. Na Inamtosheleza kuwa Ni Mjuzi wa Khabari za dhahiri na siri kuhusu dhambi za Waja Wake.

 

 

 

الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ الرَّحْمَـٰنُ فَاسْأَلْ بِهِ خَبِيرًا ﴿٥٩﴾

59. Ambaye Ameumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake katika siku sita, kisha Akawa juu[17]  ya ‘Arsh. (Yeye ni) Ar-Rahmaan, basi ulizia kuhusu Yeye, kwani Ni Mjuzi wa Khabari za dhahiri na siri.

 

 

 

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اسْجُدُوا لِلرَّحْمَـٰنِ قَالُوا وَمَا الرَّحْمَـٰنُ أَنَسْجُدُ لِمَا تَأْمُرُنَا وَزَادَهُمْ نُفُورًا ۩﴿٦٠﴾

60. Na wanapoambiwa: Msujudieni Ar-Rahmaan husema: Ni nani huyo Ar-Rahmaan? Tumsujudie unayetuamrisha, na inawazidishia kukengeuka kwa chuki.[18]

 

 

تَبَارَكَ الَّذِي جَعَلَ فِي السَّمَاءِ بُرُوجًا وَجَعَلَ فِيهَا سِرَاجًا وَقَمَرًا مُّنِيرًا ﴿٦١﴾

61. Amebarikika Ambaye Amejaalia buruji[19] katika mbingu na Amejaalia humo taa yenye mwanga mkali na mwezi wenye nuru.

 

 

 

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ خِلْفَةً لِّمَنْ أَرَادَ أَن يَذَّكَّرَ أَوْ أَرَادَ شُكُورًا ﴿٦٢﴾

62. Naye Ndiye Aliyejaalia usiku na mchana ufuatane kwa atakaye kukumbuka au atakaye kushukuru.

 

 

 

وَعِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ الْجَاهِلُونَ قَالُوا سَلَامًا ﴿٦٣﴾

63. Na Waja wa Ar-Rahmaan[20] ni wale wanaotembea katika ardhi kwa unyenyekevu na upole, na majahili wanapowasemesha, wao husema: Salaamaa (amani)!

 

 

 

وَالَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمْ سُجَّدًا وَقِيَامًا ﴿٦٤﴾

64. Na wale wanaokesha usiku kwa ajili ya Rabb wao wakisujudu na kusimama.[21]

 

 

 

وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا اصْرِفْ عَنَّا عَذَابَ جَهَنَّمَ ۖ إِنَّ عَذَابَهَا كَانَ غَرَامًا ﴿٦٥﴾

65. Na wale wanaosema: Rabb wetu! Tuepushe adhabu ya Jahannam. Hakika adhabu yake ni yenye kugandamana daima; isiyomwacha mtu.

 

 

 

إِنَّهَا سَاءَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا ﴿٦٦﴾

66. Hakika hiyo (Jahannam) ni mahali paovu mno pa kustakiri na mahali pa kuishi.

 

 

وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا ﴿٦٧﴾

67. Na wale ambao wanapotoa huwa hawafanyi israfu[22] na wala hawafanyi uchoyo na wanakuwa wastani baina ya hayo.

 

 

 

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا ﴿٦٨﴾

68. Na wale ambao hawaombi pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine na wala hawaui nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na wala hawazini. Na atakayefanya hivyo atakutana na adhabu.

 

 

 

يُضَاعَفْ لَهُ الْعَذَابُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِ مُهَانًا ﴿٦٩﴾

69. Ataongezewa adhabu maradufu Siku ya Qiyaamah, na atadumu humo akidhalilishwa.

 

 

 

إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٠﴾

70. Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akatenda amali njema. Basi hao Allaah Atawabadilishia maovu yao kuwa mema. Na Allaah daima Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu.

 

 

 

وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَإِنَّهُ يَتُوبُ إِلَى اللَّـهِ مَتَابًا ﴿٧١﴾

71. Na atakayetubu na akatenda mema, basi hakika yeye anatubia kwa Allaah tawbah ya kweli.[23]

 

 

 

وَالَّذِينَ لَا يَشْهَدُونَ الزُّورَ وَإِذَا مَرُّوا بِاللَّغْوِ مَرُّوا كِرَامًا ﴿٧٢﴾

72. Na wale ambao hawashuhudii uongo, na wanapopita kwenye upuuzi hupita kwa heshima.

 

 

 

وَالَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ لَمْ يَخِرُّوا عَلَيْهَا صُمًّا وَعُمْيَانًا ﴿٧٣﴾

73. Na wale ambao wanapokumbushwa Aayaat za Rabb wao, hawapinduki kuzifanyia uziwi na upofu.

 

 

 

 

وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

74. Na wale wanaosema: Rabb wetu! Tutunukie katika wake zetu na dhuria wetu viburudisho vya macho yetu, na Tujaalie kuwa waongozi kwa wenye taqwa.

 

 

 

أُولَـٰئِكَ يُجْزَوْنَ الْغُرْفَةَ بِمَا صَبَرُوا وَيُلَقَّوْنَ فِيهَا تَحِيَّةً وَسَلَامًا ﴿٧٥﴾

75. Hao ndio watakaolipwa maghorofa ya juu (Jannah) kwa kuwa walisubiri, na watapokelewa humo kwa maamkizi na amani.

 

 

 

خَالِدِينَ فِيهَا ۚ حَسُنَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا ﴿٧٦﴾

76. Wadumu humo. Uzuri ulioje wa mahali pa kustakiri na makazi ya kuishi daima!

 

 

 

قُلْ مَا يَعْبَأُ بِكُمْ رَبِّي لَوْلَا دُعَاؤُكُمْ ۖ فَقَدْ كَذَّبْتُمْ فَسَوْفَ يَكُونُ لِزَامًا ﴿٧٧﴾

77. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Rabb wangu Asingekujalini lau kama si duaa zenu. Kwa yakini mmekadhibisha, basi adhabu itakuwa ya lazima kukugandeni tu!

 

 

 

 

 

[1] Maana ya Al-Furqaan: Pambanuo

 

Maana ya Furqaan kilugha ni kupambanua baina ya vitu viwili.

 

Ama kiistilahi, ni kupambanua baina ya haki na batili. Hivyo basi, ni kupambanua baina ya hidaaya na upotofu, baina ya imaan na kufru, baina ya shirki na Tawhiyd, baina ya Sunnah na bid’ah n.k.

 

Neno hili limetajwa katika Suwrat Al-Baqarah Aayah (2:53), (2:185). Na katika Al-Anfaal (8:41), imemaanishwa kupambanua baina ya makundi mawili; ya Waislamu na makafiri katika vita vya Badr. Hali kadhaalika, Furqaan imetajwa katika Al-Anbiyaa (21:48). Na inamaanisha pia baswiyrah (nuru za ilimu, utambuzi, umaizi) ambayo inapambanua baina yake na baina ya yaliyo kinyume chake, ambayo ni viza, ujinga, ujahili n.k.

 

[2] Kufru Za Washirikina Kumkanusha,  Kumsingizia, Kumpachika  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) Sifa Kadhaa Ovu, Kumfanyia Istihzai Yeye Pamoja Na Kuifanyia Istihzai Qur-aan Na Kuikanusha:

 

Kuanzia Aayah hii namba (4) hadi namba (8), Allaah (سبحانه وتعالى) Anataja kufru za washirikina kumkanusha Rasuli Wake  (صلى الله عليه وآله وسلم), na kumsingizia, na kumpachika sifa ovu kadhaa. Na kwa ujumla, sifa ovu walizomsingizia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni zifuatazo: 

 

(i)  Mchawi:

 

Rejea Yuwnus (10:2), Al-Israa (17:47), Al-Anbiyaa (21:3), Suwrah hii Al-Furqaan (25:8), Swaad (38:4), Al-Muddath-thir (74:25).

 

(ii)  Kuhani:

 

Rejea Al-Anbiyaa (21:5), Atw-Twuwr (52:30).

 

(iii) Mshairi:

 

Rejea Al-Hijr (15:6), Al-Muuminuwn (23:70), Asw-Swaaffaat (37:36), Ad-Dukhaan (44:14), Al-Qalam (68:51).

 

(iv) Majnuni na muongo:

 

Rejea Saba-a (34:8), Swaad (38:4). 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Anawaraddi hao kwa Kauli Zake kwenye Al-A’raaf (7:184), Atw-Twuwr (52:29), Al-Haaqqah (69:40-43), Saba-a (34:46), Yaasiyn (36:70), Al-Qalam (68:2), At-Takwiyr (81:22).

 

Na kufru kama hizo pia zilikuwa za washirikina na makafiri wa awali, ambao nao waliwakanusha Rusuli (Mitume) wao kwa kauli kama hizo. Allaah (سبحانه وتعالى) Anathibitisha hayo katika Kauli Zake kadhaa kama katika Suwrah Adh-Dhaariyaat (51:52).

 

Na katika kuisingizia Qur-aan, kuifanyia istihzai na kuikanusha, madai yao yalikuwa kama ifuatavyo:

 

(i) Ameibuni, ameitunga, ni hekaya za awali, ndoto za mkorogano:

 

Rejea Aayah hii ya Al-Furqaan (25:4), (6), Al-Anbiyaa (21:5), Atw-Twuwr (52:30).

 

Rejea pia Sababun-Nuzuwl (Sababu Ya Kuteremshwa) Aayah katika Suwrah An-Nahl (16:103):

 

(ii) Ni Sihri (uchawi):

 

Rejea Al-An’aam (6:7), Al-Anbiyaa (21:3), Saba-a (34:42), Asw-Swaaffaat (37:15), Az-Zukhruf (43:30), Al-Ahqaaf (46:7), Al-Qamar (54:2), Al-Muddath-thir (74:24).

 

Lakini Allaah (سبحانه وتعالى) Anaraddi kauli za hao makafiri na washirikina za kuikanusha na kuisingizia Qur-aan  katika Kauli Zake mbalimbali. Miongoni mwazo ni katika Suwrah hii ya Al-Furqaan Aayah namba (6) kwamba Ameiteremsha Yeye Qur-aan; Muumba wa mbingu na ardhi na Mjuzi wa siri.

 

Na kwengineko kwingi katika Qur-aan, Allaah (سبحانه وتعالى) Ametaja aina kama hizo za kufru zao washirikina na makafiri, wa awali na wa zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) za kukanusha Rusuli Wake (عليهم السّلام) na kupinga Vitabu Vyake Vitukufu Alivyoviteremsha.  

 

[3] Washirikina Kudai Waletewe Asiyekuwa Binaadam:

 

Hizi ni katika kauli za wakanushaji wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ambazo kwazo walitilia doa Risala yake. Walipinga kwa kuuliza kwa nini asiwe ni Malaika au mfalme, au kwa nini Malaika hakuteremshwa kumsaidia, wakasema:

  مَالِ هَـٰذَا الرَّسُولِ  

“Ni Rasuli gani huyu?”

 

Yaani: Ni nani huyu anayedai Urasuli? Wamesema hivyo kukusudia dhihaka na kumfanyia istihzai.

 

Wakasema pia:

  يَأْكُلُ الطَّعَامَ  

“Anakula chakula.”

 

Ilhali hii ni sifa mojawapo ya wanaadam. 

 

Wakadai: Kwa nini asitumwe Malaika ambaye hali chakula na hahitaji mambo wanayoyahitajia wanaadam?

 

Wakaendelea kusema:

  وَيَمْشِي فِي الْأَسْوَاقِ ۙ  

“Na anatembea masokoni!”

 

Yaani:  Kuuza na kununua.

 

Kwa mujibu wa madai yao, wamekusudia kuwa hayafai haya kwa Rasuli ilhali Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

وَمَا أَرْسَلْنَا قَبْلَكَ مِنَ الْمُرْسَلِينَ إِلَّا إِنَّهُمْ لَيَأْكُلُونَ الطَّعَامَ وَيَمْشُونَ فِي الْأَسْوَاقِ ۗ

“Na Hatukupeleka kabla yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Rusuli wowote isipokuwa bila shaka wakila chakula, na wanatembea masokoni. [Al-Furqaan (25:20)] 

 

Wakaendelea kusema:

  لَوْلَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مَلَكٌ  

“Kwa nini asiteremshiwe Malaika.”

 

Yaani: Kwa nini asiteremshwe Malaika pamoja naye kumsaidia?

فَيَكُونَ مَعَهُ نَذِيرًا ﴿٧﴾

“Akawa muonyaji pamoja naye? “

 

Kutokana na madai yao, wamekusudia kwamba Rasuli hatoshelezi kubalighisha Risala (Ujumbe) na hakuwa na uwezo wa kutekeleza Risala. [Tafsiyr As-Sa’diy]

 

Rejea pia Al-Israa (17:90-94) kwenye madai kama hayo ya washirikina kutaka wateremshiwe asiyekuwa binaadam.

 

Pia Allaah (سبحانه وتعالى) Ametaja kufru zao hizo katika Aayah nyenginezo na Akaraddi kauli zao. Rejea katika Suwrah hii Al-Furqaan (25:20), na rejea pia Al-An’aam (6:8-9) na Al-Anbiyaa (21:8). Na Akawaraddi Manaswara pia waliomfanya Nabii wao kuwa ni mwabudiwa. Rejea Al-Maaidah (5:75).

 

Na makafiri wa awali pia waliwakanusha Rusuli wao kwa madai kama hayo. Rejea Al-Muuminuwn (23:33-34) kujua baadhi ya kufru zao.

 

[4]  Majaribio (Na Mitihani) Baina Ya Watu:

 

Rasuli anakuwa ni majaribio na mtihani kwa watu ambao ametumwa kuwafikishia Ujumbe. Ni majaribio na mtihani pia kwa watakaomkubali (wabebe makalifisho) na watakaomkataa (wafanye watakavyo wao). Na Rusuli wote Allaah Aliwapa mtihani na majaribio ya kuwalingania watu.

 

Na tajiri ni jaribio na mtihani kwa maskini, na maskini pia ni jaribio na mtihani kwa tajiri na kadhalika. Aina zote za watu hapa duniani ni majaribio na mtihani baina yao, kwani dunia ni nyumba ya fitnah, majaribio na mitihani. [Tafsiyr As-Sa’diy].

 

Kuhusu kauli ya kwanza iliyotangulia katika Aayah hii kuwa Rusuli wote walikuwa ni binaadam wanaokula na kunywa, rejea Suwrah hii Al-Furqaan Aayah namba (7).

 

[5] Kufru Za Washirikina Kutaka Ateremshwe Malaika Na Wamuone Allaah:

 

Rejea Al-Israa (17:90-93).

 

[6] Marufuku Kwa Washirikina Na Makafiri Kupata Mafanikio:

 

Siku watakapowaona Malaika wakati wa kufariki kwao, na wakiwa ndani ya makaburi yao, na Siku ya Qiyaamah, kwa sura ambayo siyo ile waliyoitaka. Sio kuwapa bishara ya Jannah (Pepo), lakini kuwaambia: “Allaah Ameifanya Jannah ni mahali palipoharamishwa kwenu.” [Tafsiyr Al-Muyassar]

 

[7] Amali  Ambazo Hazina Dalili Ni Batili Hivyo Hazipokelewi:

 

Rejea Al-Kahf (18:103), Az-Zumar (39:65).

 

[8] Malaika Na Allaah Watateremka Siku Ya Qiyaamah:

 

Rejea Al-Haaqqah (69:13-18), Al-Fajr (89:21-22), Al-Baqarah (2:210), Al-An’aam (6:158).

 

Ikumbuke ee Rasuli! Siku hiyo ambayo mbingu zitapasukapasuka, na yatatokeza kupitia mianya ya mipasuko yake mawingu meupe yaliyo membamba. Na Siku hiyo, Allaah (سبحانه وتعالى) Atawateremsha Malaika wa mbinguni wawazunguke viumbe katika sehemu walipokusanywa wote (mahshar), na kisha Aje Allaah (تبارك وتعالى), ujio unaolingana na Utukufu Wake, kuwahukumu waja. [Tafsiyr Al-Muyassar]

 

[9] Majuto Ya Mtu Kwa Kumfuata Shaytwaan Na Watu Waovu:

 

Aayah hii hadi namba (29), zinataja jinsi mtu anavyojuta kwa kutokumfuata Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na badala yake akamfuata shaytwaan na rafiki muovu.

Tafsiyr za Aayah hizo:  

 

Na ikumbuke ee Rasuli! Siku ambayo mwenye kujidhulumu nafsi yake ataiuma mikono yake kwa majuto na maunguliko kwa kusema: “Laiti mimi niliandamana na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na nikamfuata katika kuufanya Uislamu kuwa ni njia ya Peponi.” Na atasema kwa maunguliko: “Laiti mimi sikumfanya fulani kuwa ni rafiki mwandani wa kumfuata na kumpenda. Amenipoteza rafiki huyu na kuniepusha na Qur-aan baada ya kunijia.” Na shaytwaan aliyefukuzwa kwenye Rehma ya Allaah amekuwa daima ni mwenye kumtupa na kumwacha mkono mwanaadam.

 

Katika Aayah hizi, kuna onyo kwamba rafiki mbaya asifuatwe, kwani yeye huenda akawa ni sababu ya kumtia motoni yule anayefuatana naye. [Tafsiyr Al-Muyassar].

 

Rejea pia Asw-Swaaffaat (37:50-57) ambako rafiki aliyeepukana na rafiki muovu akaingizwa Peponi, anashukuru kutokumfuata rafiki muovu aliyekuwa motoni kwa kuwa alitaka   kumpotosha.   

 

Na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amenasihi kufuatana na rafiki mwema na kuepukana na rafiki muovu akapiga mfano baina yao:

 

عَنْ أَبِي مُوسَى الأَشْعَرِيِّ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((إِنَّمَا مَثَلُ الْجَلِيسِ الصَّالِحِ وَالسَّوْءِ كَحَامِلِ الْمِسْكِ وَنَافِخِ الْكِيرِ. فَحَامِلُ الْمِسْكِ إِمَّا أَنْ يُحْذِيَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَبْتَاعَ مِنْهُ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ مِنْهُ رِيحًا طَيِّبَةً. وَنَافِخُ الْكِيرِ إِمَّا أَنْ يُحْرِقَ ثِيَابَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ مِنْهُ  رِيحًا مُنْتِنَةً)) متفق عليه

 

Amesimulia Abuu Muwsaa Al-Ash-‘ariyyi (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika mfano wa mtu mwema anayekaa na watu, na mtu mwovu anayekaa na watu, ni kama mfano wa mbebaji miski na (mfua chuma) anayevuvia kipulizo. Mbebaji miski, ima atakupa, au utanunua kutoka kwake, au utapata harufu nzuri kwake. Ama anayevuvia kipulizo, ima atachoma nguo zako, au utapata harufu mbaya kutoka kwake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

[10] Kuihama Qur-aan Ni Kuipuuza Na Kutokufuata Yaliyoamrishwa:

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwita Rabb wake kumlalamikia na kumsikitikia kupuuzwa na watu wake katika yale aliyoyaleta.  Akasema: Ee Rabb wangu! Hakika watu wangu ambao Umenituma kwao ili niwaongoze na kuwabalighishia Risala, wameihama hii Qur-aan. Yaani: Wameipuuza, wameikwepa, na wakaiacha ilhali wajibu ulio juu yao ni kuzitii hukmu zake, kuzitekeleza sharia zake na kuyafuata yote yaliyomo ndani yake. [Tafsiyr As-Sa’diy].

 

Kuihama pia inamaanisha kuipuuza kwa kutokuisoma, kwani baadhi ya Salaf wamefafanua maana ya watu kuihama na kupuuza Qur-aan kama ifuatavyo:

 

(i)    Wasioisoma kabisa.

(ii)   Wanaoisoma lakini hawajifunzi maana yake.

(iii) Wanaoisoma na kujifunza maana yake lakini hawafuati maamrisho yake na hawajiepushi na makatazo yake.

 

[11] Hikma Ya Qur-aan Kuteremshwa Kidogo Kidogo

 

Rejea Alhidaaya.com: Hikmah Ya Kuteremshwa Qur-aan Kidogo Kidogo Wakati Mbali Mbali

 

[12] Makafiri Watakusanywa Juu Ya Nyuso Zao Waelekee Jahannam:

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ مُحَمَّدٍ، حَدَّثَنَا يُونُسُ بْنُ مُحَمَّدٍ الْبَغْدَادِيُّ، حَدَّثَنَا شَيْبَانُ، عَنْ قَتَادَةَ، حَدَّثَنَا أَنَسُ بْنُ مَالِكٍ ـ رضى الله عنه أَنَّ رَجُلاً، قَالَ يَا نَبِيَّ اللَّهِ كَيْفَ يُحْشَرُ الْكَافِرُ عَلَى وَجْهِهِ قَالَ ‏ "‏ أَلَيْسَ الَّذِي أَمْشَاهُ عَلَى الرِّجْلَيْنِ فِي الدُّنْيَا قَادِرًا عَلَى أَنَّ يُمْشِيَهُ عَلَى وَجْهِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ‏"‏‏.‏ قَالَ قَتَادَةُ بَلَى وَعِزَّةِ رَبِّنَا‏.‏

Amesimulia Qataadah (رضي الله عنه):  Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema: Mtu mmoja alisema: Ee Nabii wa Allaah! Vipi kafiri atakusanywa juu ya uso wake?  Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Je, kwani Yule Aliyemfanya kutembea kwa miguu yake duniani Hana uwezo wa kumfanya atembee kwa uso wake Siku ya Qiyaamah?” Qataadah amesema: “Bali Naam! Kwa Utukufu wa Rabb wetu.”  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Rejea pia Al-Israa (17:97).

 

[13] Watu Wa Ar-Rass:

 

Ar-Rass imesemekana kuwa ni kisima kwa mujibu wa Tafsiyr ya Ibn Kathiyr. Lakini kuhusu watu wa Ar-Rass, ‘Ulamaa wamekhitilafiana. Na hakuna dalili iliyothibiti kuelezewa ni watu gani. Hivyo basi, Rasuli aliyetumwa kwa watu hao, ni miongoni mwa Rusuli ambao Allaah (سبحانه وتعالى) Hakuwasimulia visa vyao kama Anavyosema katika Suwrah Ghaafir (40:78) na An-Nisaa (4:164). Naye Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Awajuaye zaidi. Imetajwa Watu wa Ar-Rass katika Suwrah hii na katika Qaaf (50:12).

 

[14] Hawaa (Matamanio) Ya Mtu Kuwa Ndio Mwabudiwa:

 

Uislamu ni kujisalimisha kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa utii. Ina maana: Mja asiwe na mashaka yoyote kuhusu Amri za Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم). Na pia akubali kwa kuridhia Amri za Rabb Wake na amri za Rasuli Wake katika vipengele vyote vya maisha. Huu ndio msingi wa Uislamu. Yeyote atakaepinga  Sharia za Allaah kwa maoni yake, basi atakuwa  hakujisalimisha kwa Allaah, bali yeye ni mtumwa tu wa hawaa (matamanio) zake, na yeye ndie yule aliyekusudiwa katika Kauli hii ya Allaah (سبحانه وتعالى):

أَرَأَيْتَ مَنِ اتَّخَذَ إِلَـٰهَهُ هَوَاهُ  

“Je, umemuona yule aliyefanya hawaa yake kuwa ndio mwabudiwa wake?” 

 

Na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ameonya:

 

عَنْ أَبِي مُحَمَّدٍ عَبْدِ اللَّهِ بِنْ عَمْرُو بِنْ العَاصِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا  قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وآله وسلم: ((لا يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يَكُونَ هَوَاهُ تَبَعَاً لِمَا جِئْتُ بِهِ)) حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ، رَوَيْنَاهُ فِي كِتَابِ  الْحُجَّةِ  بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ.

Amesimulia Abuu Muhammad ‘Abdillaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hatoamini mmoja wenu mpaka hawaa (matamanio) zake zitakapomili kutii yale niliyokuja nayo.” [Hadiyth Hasan Swahiyh, katika Kitabu “Al-Hujjah” kwa Isnaad Swahiyh]

 

Rejea pia Al-Jaathiyah (45:23).

 

[15] Allaah (سبحانه وتعالى) Anahuisha Ardhi Iliyokufa; Ni Kama Mfano Wa Kufufuliwa Watu:

 

Rejea Al-An’aam (6:95), Ar-Ruwm (30:50), Yaasiyn (36:33).

 

[16] Bahari Mbili; Tamu Na Ya Chumvi Kukutana Bila Kuchanganyika:

 

Rejea Ar-Rahmaan (55:19-21).

 

[17] Istawaa اسْتَوَى

 

Yuko juu kwa namna inayolingana na Uadhama na Ujalali Wake Yeye Mwenyewe Allaah (سبحانه وتعالى). Rejea Al-A'raaf (7:54) kwenye maelezo bayana ya maana yake, yenye kutofautiana na maana ya katika Suwrah Al-Baqarah (2:29) na Suwrat Fusswilat (41:11).

 

[18]  Makafiri Walipinga Jina La Ar-Rahmaan:

 

Rejea Al Israa (17:110) ambapo kumetajwa sababu ya kuteremshwa Aayah kuhusiana na haya.

 

[19] Maana Ya Buruji:

 

‘Ulamaa wana rai kadhaa kuhusu maana ya buruji. Rejea Al-Buruwj (85:1) kwenye maelezo bayana ya maana yake.  

 

[20] Waja Wa Ar-Rahmaan Na Sifa Zao:

 

Kuanzia Aayah hii (25:63) hadi (25:76), Allaah (سبحانه وتعالى) Anataja Sifa njema za Waja Wake.

 

[21] Qiyaamul-Layl: (Kisimamo Cha Usiku) Kwa Ajili Ya Ibaada:

 

Rejea Al-Israa (17:79), As-Sajdah (32:17). Pia rejea Adh-Dhaariyaat  (51:15-19) ambapo fadhila zake zimetajwa. Rejea pia Az-Zumar (39:9), Aal-‘Imraan (3:17), (3:113) na Al-Muzzammil: (73:2).

 

[22] Tofauti Kati Ya Israfu Na Ubadhirifu. Rejea Al-Israa (17:26).

 

[23] Tawbah Ya Kikweli Na Fadhila Zake:

 

Rejea Huwd (11:3) kwenye faida tele za istighfaar na tawbah. Rejea pia At-Tahriym (66:8) kwenye faida kuhusu tawbah ya kikweli na  masharti yake.

 

 

 

Share