Imaam Ibn Baaz: Hukmu Ya Anayeswali Ijumaa Pekee Na Kuacha Swalaah Zilizobaki

Hukmu Ya Anayeswali Ijumaa Pekee Na Kuacha Swalaah Zilizobaki

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Kuna mtu anaswali Ijumaa pekee bila kuswali Fardhi zilizobaki, je, inakubaliwa Swalaah yake?

 

 

JIBU:

 

Haikubaliwi Swalaah yake, kwa hakika amekuwa Kafiri kwa hilo.

 

Swalaah yake ya Ijumaa, Swawm yake, na matendo yake yote ni batili.

 

Anasema Aliyetukuka:

"Na kama wangemshirikisha bila shaka yangebatilika yale waliyokuwa wakitenda." [Al-An'aam: 88]

 

Na Anasema Aliyetakasika:

"Na yeyote atakayekufuru iymaan; basi kwa yakini zimebatilika 'amali zake; naye Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika." [Al-Maaidah: 5]

 

Basi yule anayekufuru kufru kubwa au shirki kubwa, huporomoka matendo yake.

Tunamuomba Allaah afya (Atulinde).

Na kuacha Swalaah ni kufru kubwa."

 

[Nuwr 'Alaa Ad-Darb, 13/339]

 

 

Share