Imaam Ibn Baaz: Hukmu Ya Kutikisa Kichwa Wakati Wa Kutoa Salaam

Hukmu Ya Kutikisa Kichwa Wakati Wa Kutoa Salaam

 

 www.alhidaaya.com

 

 

Aliulizwa Shaykh Ibn Baaz (Rahimahu Allaah):

 

Kuna baadhi ya watu, wakati wa kutoa salaam baina ya salaam ya kwanza na salaam ya pili (katikati ya salaam) hutikisa kichwa kuelekea chini; je, ni ipi hukmu ya hilo?

 

 

Akajibu kwa kusema:

 

Jambo hilo halina asili na ni makruhu kufanya hivyo kwani hakuna asili (dalili) juu ya hilo.

 

 

[Fataawa Nuurun 'Alaa Ad-Darb, juzuu 9, uk. 29]

 

Share