Imaam Ibn Baaz: Kubusu Mkono Au Kuweka Mkono Kifuani Baada Ya Kuamkiana

Kubusu Mkono Au Kuweka Mkono Kifuani Baada Ya Kuamkiana

 

Imaam Bin Baaz (Rahimahu-Allaah)

 

 www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Naona baadhi ya watu baada ya kupeana mikono kuamkiana wanabusu mikono yao au wanaweka mkono kifuani kudhihirisha mapezi zaidi. Je, inahurusiwa? Tunufaishe Jazaaka Allaahu khayraa.

 

 

JIBU:

 

Tunavyojua, kitendo hicho hakina asili katika Shariy’ah ya Kiislam na haikuamuriwa kubusu mkono au kuweka kifuani baada ya kupeana mikono katika kuamkiana, bali ni bid’ah ikiwa anaamini kuwa kufanya hivyo kunamkurubisha kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

 

 

[Imaam bin Baaz, Bid’ah Wa Muhdathaat Wa Maa Laa Aswla Lahaa (Uk. 477)]

 

Share