083-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Mutwaffifiyn Aayah 1-6: وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Suwrah Al-Mutwaffifiyn

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

083-Al-Mutwaffifiyn

 

 

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

 

عَنَّ عِكْرِمَة، حَدَّثَهُ عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ لَمَّا قَدِمَ النَّبِيُّ  صلى الله عليه وسلم الْمَدِينَةَ كَانُوا مِنْ أَخْبَثِ النَّاسِ كَيْلاً فَأَنْزَلَ اللَّهُ سُبْحَانَهُ: ((وَيْلٌ لِلْمُطَفِّفِينَ))‏ فَأَحْسَنُوا الْكَيْلَ بَعْدَ ذَلِكَ ‏.‏

Ikrimah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amehadithia kuwa pindi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipofika Madiynah alikuta watu wa Madiynah wakipunjiana kilo na walikuwa ni wenye tabia mbaya kabisa katika jambo hilo. Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:

 

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

Na baada ya hapo wakafanya uzuri katika kupima na kuacha tabia yao hiyo mbaya kupunja katika kipimo  [bn Maajah Kitaab At-Tijaraat (2223)]

 

Ibn Kathiyr:

 

Kuongeza na kupunguza katika kupima kwa pishi au mizani ndio sababu ya adhabu kali na kupata hasara.

 

Amepokea An-Nasaaiy na Ibn Maajah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipofika Madiynah walikuwa watu wa Madiynah ni waovu mno kuliko watu wote katika  kupunja Allaah (سبحانه وتعالى)  Akateremsha:

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

Wakapima vizuri baada ya hapo [An-Nasaaiy katika Al-Kubraa (6/508) na Ibn Maajah (2/748)]

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ﴿٢﴾

2. Ambao wanapopokea kipimo kwa watu wanataka wapimiwe kamilifu.

 

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ﴿٣﴾

3. Na wanapowapimia (watu) kwa kipimo au wanawapimia kwa mizani wanapunja.

 

أَلَا يَظُنُّ أُولَـٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ﴿٤﴾

4. Je, hawadhanii kwamba wao watafufuliwa?

 

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿٥﴾

5. Kwenye Siku adhimu.

 

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٦﴾

6. Siku watakayosimama watu kwa Rabb wa walimwengu.

 

 

Share