Rajab: Mi’raaj Imetokea Katika Rajab? Na Tarehe Gani? Na ‘Ibaada Zipi Za Kutenda?

 

Mi’raaj Imetokea Katika Rajab Na Tarehe Gani Na ‘Ibaada Zipi Za Kutenda?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Asalam alykum

 

Miraji imetokea siku gani? Na ibada gani za kutenda katika mwezi huo? Tunaomba mtufutu enyi mashekhe wetu.

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Kuhusu Mi'iraaj, watu wanafunga na kufanya mambo mengine mambo ambayo hayana dalili wala msingi katika Dini yetu tukufu. Tukio hilo ambalo lilitokea katika maisha ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) bila shaka yoyote. Lakini wana Historia wametofautiana kuhusu tarehe na haijulikani kihakika ni gani japokuwa wengine wamechukua ni 27 Rajab, na wengine wametaja miezi na tarehe tofauti na hiyo. Wakati huo hata Swawm yenyewe ilikuwa haijafaradhishwa kwa Waislam. Wala hakuna ‘ibaada yoyote iliyothibiti kutendwa katika mwezi huu isipokuwa tu Rajab ni miongoni mwa miezi mitukufu basi linalopasa ni kukithirisha ‘amali njema na kila aina za ‘ibaadah kujichumia thawabu nyingi.

 

Kwa maelezo zaidi na faida bonyeza viungo vifuatavyo:

 

Rajab: Uzushi Wa Kuomba Maghfirah Katika Mwezi Wa Rajab

Rajab: Hakuna ‘Ibaadah Maalumu, Swawm, Wala Du’aa Makhsusi Kwa Ajili Ya Mwezi Wa Rajab

Rajab: Kufunga (Swawm) Na Kusherehekea Siku Inayosemekana Ni Ya Israa na Mi'iraaj

Rajab: Swawm Katika Mwezi Wa Rajab Ipi Ni Sunnah; Kufunga Mwezi Mzima Au Siku Maalumu?

Rajab: Fadhila Za Mwezi Wa Rajab Na Yaliyozuliwa Ndani Yake

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

  

 

 

Share