62-Malaika: Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini: (10)– Malaika Wanateremka Wakati Muumini Anasoma Qur-aan

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

62:   Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini  

 

(10)– Malaika Wanateremka Wakati Muumini Anasoma Qur-aan

 

Hali hii inatokea pale Muumini anapoisoma Qur-aan kwa ikhlaas na tartiyl makini, anapohudhurisha moyo wake, anapoizingatia ipasavyo, na anapokuwa mnyenyekevu kwayo. 

 

Toka kwa Al-Baraa bin ‘Aazib (Radhwiya Allaah ‘anhu):

 

"قَرَأَ رَجُلٌ الْكَهْفَ وَفِي الدَّارِ دَابَّةٌ، فَجَعَلَتْ تَنْفِرُ فَنَظَرَ فَإِذَا ضَبَابَةٌ أَوْ سَحَابَةٌ قَدْ غَشِيَتْهُ، قَالَ: فَذَكَرَ ذَلِكَ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ:‏ اقْرَأْ فُلاَنُ، فَإِنَّهَا السَّكِينَةُ تَنَزَّلَتْ عِنْدَ الْقُرْآنِ أَوْ تَنَزَّلَتْ لِلْقُرْآنِ"

“Mtu mmoja alisoma Al-Kahf, na nyumbani kwake alikuwepo farasi, farasi akaanza kuchacharika.  Mtu yule akaangalia, na ghafla akaona wingu limemfunika.  Kisha akaenda kumweleza Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Rasuli akamwambia: Laiti ungeendelea kusoma, kwa kuwa hao walikuwa ni Malaika waliojawa utulivu, nao huteremka kwa kuandamana wakati Qur-aan inasomwa, au wanateremka kwa ajili ya Qur-aan.”  [Swahiyh Muslim: (795)].

 

Abul ‘Abbaas Al-Qurtubiy amesema:  “Neno السكينةُ katika Hadiyth, ni jina la Malaika, na wameitwa hivyo kutokana na utulivu wao wa hali ya juu wa kukiheshimu kisomo pamoja na Qur-aan yenyewe”. 

 

 

Share