68-Malaika: Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini: (16)– Wanamfunika Aliyekufa Kishahidi Kwa Mbawa Zao

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

68:   Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini  

 

(16)– Wanamfunika Aliyekufa Kishahidi Kwa Mbawa Zao

 

Imepokelewa toka kwa Jaabir (Radhwiya Allaah ‘anhu) akisema: 

 

"جيءَ بِأَبِي إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَقَدْ مُثِّلَ بِهِ وَوُضِعَ بَيْنَ يَدَيْهِ، فَذَهَبْتُ أَكْشِفُ عَنْ وَجْهِهِ، فَنَهَانِي قَوْمِي، فَسَمِعَ صَوْتَ صَائِحَةٍ فَقِيلَ ابْنَةُ عَمْرٍو، أَوْ أُخْتُ عَمْرٍو‏.‏ فَقَالَ: ‏"‏ لِمَ تَبْكِي أَوْ لاَ تَبْكِي، مَا زَالَتِ الْمَلاَئِكَةُ تُظِلُّهُ بِأَجْنِحَتِهَا"

 

“(Maiti ya) baba yangu ililetwa kwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hali ya kuwa imefanyiwa ukatili na ikawekwa mbele yake.  Nikajaribu kuikaribia ili niufunue uso wake lakini jamaa zangu walinikataza.  Rasuli akasikia sauti ya mwanamke ambaye ima ni binti ya ‘Amri au dada ya ‘Amri akilia kwa sauti ya kuomboleza, akauliza:  Kwa nini analia (au usilie)?  Malaika bado wanaendelea kumwekea kivuli kwa mbawa zao”.  [Swahiyh Al-Bukhaariy (2816)]

 

Abul ‘Abbaas Al-Qurtwubiy amesema:  “Kitendo hicho cha Malaika cha kumfunika kwa mbawa zao, kinamaanisha kwamba wanamkusanyikia na kusongana kwa shahidi huyo ili wapate kukutana naye na kupanda juu pamoja na roho yake takatifu, lakini pia kumpa bishara njema kwa yanayomsubiri mbele ya Allaah kati ya mambo mazuri na daraja za juu kabisa”.

 

 

Share