69-Malaika: Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini: (17)– Malaika Waliokuja Na Kasha Lenye Utulivu Ndani Yake

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

 

 

69:   Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini  

 

(17)– Malaika Waliokuja Na Kasha Lenye Utulivu Ndani Yake

 

 

Allaah Ta’aalaa Anasema:

 

 "وَقَالَ لَهُمْ نَبِيُّهُمْ إِنَّ آيَةَ مُلْكِهِ أَن يَأْتِيَكُمُ التَّابُوتُ فِيهِ سَكِينَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَبَقِيَّةٌ مِّمَّا تَرَكَ آلُ مُوسَىٰ وَآلُ هَارُونَ تَحْمِلُهُ الْمَلَائِكَةُ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لَّكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ "

 

“Nabiy wao akawaambia:  Hakika ishara ya ufalme wake ni kwamba litakujieni kasha ndani yake mna kituliza nyoyo kutoka kwa Rabb wenu na mabaki katika yale waliyoacha watu wa Muwsaa na watu wa Haaruwn, watalibeba Malaika. Hakika katika hayo mna ishara kwenu mkiwa ni Waumini”.  [Al-Baqarah: 248]

 

As- Sa‘adiy amesema:  “Nabiy wao aliwaelezea vile vile muujiza wa kihisia ambao wataushuhudia.  Muujiza huu ni kuletwa kasha ambalo walilipoteza muda mrefu uliopita ambapo ndanimwe kuna utulivu wa kuzipooza nyoyo na akili zao, lakini pia kuna mabaki katika yale waliyoacha watu wa Muwsaa na watu wa Haaruwn.  Malaika wakaja nalo wakiwa wamelibeba na wao wanaliona wazi wazi”.

 

 

Share