74-Malaika: Wanachopaswa Waumini Kukitenda Kwa Ajili Ya Malaika: (02)- Kuwapenda Wote Bila Kubagua

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

74:   Wanachopaswa Waumini Kukitenda Kwa Ajili Ya Malaika  

 

(02)- Kuwapenda Wote Bila Kubagua

 

Muislamu anatakiwa awapende Malaika wote kwa daraja sawa, asipambanue kati ya Malaika na Malaika, wote hao ni Waja wa Allaah.  Mayahudi wamedai kwamba kuna baadhi ya Malaika ambao ni vipenzi kwao na wengine ni maadui kwao.  Wamedai kwamba Jibriyl (‘alayhis salaam) ni adui yao, na Miykaaiyl ni kipenzi chao.  Allaah Amewajibu madai yao haya Akisema:

 

"قُلْ مَن كَانَ عَدُوًّا لِّجِبْرِيلَ فَإِنَّهُ نَزَّلَهُ عَلَىٰ قَلْبِكَ بِإِذْنِ اللَّـهِ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ وَهُدًى وَبُشْرَىٰ لِلْمُؤْمِنِينَ مَن كَانَ عَدُوًّا لِّلَّـهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَرُسُلِهِ وَجِبْرِيلَ وَمِيكَالَ فَإِنَّ اللَّـهَ عَدُوٌّ لِّلْكَافِرِينَ "

 

“Sema:  Yeyote aliyekuwa adui wa Jibriyl, basi hakika yeye ameiteremsha Qur-aan katika moyo wako (ee Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) kwa Idhini ya Allaah inayosadikisha yaliyo kabla yake, na mwongozo na bishara kwa Waumini. ●. Yeyote aliyekuwa adui wa Allaah na Malaika Wake, na Rusuli Wake, na Jibriyl, na Miykaala, basi hakika Allaah Ni adui kwa makafiri”.  [Al-Baqarah: 97-98]

 

 

Share