44-Tukumbushane: Vipi Kuhusu Paka Na Nyani?

 

Tukumbushane

 

Alhidaaya.com

 

 

 

44:  Vipi Kuhusu Paka Na Nyani?

 

Wawili hawa ni haramu kuwala.

 

Kuhusu nyani, Al-Imaam bin Qudaamah amesema kwenye Al-Mughniy:  “Kula nyani hairuhusiwi, na haijuzu pia kumuuza”.

 

Ibn ‘Abdul Barri pia kasema:  “Hakuna  mvutano wowote ujulikanao baina ya ‘Ulamaa kuhusiana na kutojuzu kula nyama ya nyani au kuiuza”.

 

Sababu ya kuharamishwa nyani, ni kwa kuwa ana meno makali, aliwahi kubadilishwa sura na kuwa mbaya, na ni katika wanyama wabaya.

 

Ama paka, yeye ni haramu kwa vile ana meno na kucha.  Na kwa msingi huo, anaingia yeye pamoja na nyani kwenye kundi la wanyama wenye meno makali na ndege wenye kucha kali kwa mujibu wa Hadiyth ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) iliyotajwa nyuma.

 

Sokwe, tumbili na mfano wao wanaingia kundi la nyani.

 

 

Share