19-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Posa Na Hukumu Zake:Je, Mwanamke Naye Anaruhusiwa Kumwangalia Mwanaume

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

 

 

الخِطْبَةُ وأَحْكَامُهَا

 

Posa Na Hukumu Zake

 

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

19:   Je, Mwanamke Naye Anaruhusiwa Kumwangalia Mwanaume?:

 

Hukmu ya mwanamke kumwangalia aliyemposa ni sawa na hukmu ya mwanaume kumwangalia yeye, kwa kuwa yanayompendeza kutoka kwa mwanaume ni yale yale yanayompendeza mwanaume kutoka kwake.  Hili ni muhimu zaidi kwa mwanamke, kwa sababu mwanaume ana uwezo wa kumwacha mwanamke kama hakumpendeza baada ya kumwoa kinyume na mwanamke.

 

Hapa kiufupi tunaweza kusema kwamba sharia haikumwelekeza mwanamke kumwangalia aliyemchumbia, kwa kuwa wanaume ni rahisi kuwaona katika jamii, hawafichiki kama wanavyofichikana wanawake.  Mwanamke anaweza kwa urahisi kumwona mwanaume aliyemposa.  Na mpaka wa kumwangalia ni zaidi ya uso na viganja isipokuwa kati ya kitovu na magoti, sehemu hiyo ndio uchi wa mwanaume.

 

 

Share