13-Majini: Aina Za Majini Kutokana Na Maumbo Yao
Majini
13- Aina Za Majini Kutokana Na Maumbo Yao
Toka kwa Abu Tha’alabah Al-Khushaniy (Radhwiya Allaah ‘anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
"الجِنُّ ثَلاثةُ أصنافٍ: صِنْفٌ لَهم أجنِحةٌ يَطيرونَ في الهَواءِ، وصِنفٌ حَيَّاتٌ وكِلابٌ، وصِنْفٌ يَحلُّونَ ويَظعَنونَ"
“Majini ni sampuli tatu: Sampuli ya wenye mbawa ambao wanaruka hewani, sampuli ya nyoka na mbwa, na sampuli ya wanaokaa sehemu na kusafiri”. [Ni swahiyh. Iko katika Mishkaat Al Maswaabiyh (4148)]
