Biskuti Za Tende

Biskuti Za Tende

 

 

 

 

 VIPIMO

 
Unga -  4 Vikombe vya chai
Sukari ya laini  (icing sugar) - 1 Kikombe cha chai
Baking powder -  2 Vijiko vya chai
Mayai  -   2
Siagi au margarine -  1 Kikombe cha chai
Vanilla -1 Kijiko cha chai
Maziwa ya kuchanganyia - kiasi
Tende iliyotolewa koko -  1 Kikombe

ufuta (sasame) kiasi  1/4  kikombe

 

Namna Ya  Kutayarisha Na Kupika

  1. Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika mashine.
  2. Kisha tia mayai, vanilla na halafu maziwa kidogo kidogo hadi mchanganyiko ushikamane.
  3. Gawanya madonge mawili na usukume kama chapati, lakini sio nyembamba sana.
  4. Tandaza tende robo ya duara na unyunyize ufuta duara zima: kisha kunja hadi mwisho na ukate kate, kisha upange katika trei ya kuvumbika.
  5. Vumbika (bake)  moto wa 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi vigeuke rangi na viwive.
  6. Zikisha iiva ziache zipowe na zitakuwa tayari kuliwa.

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 


 

 

 

  

 

Share