05-Wasifu Wa Maswahaba Kumi Waliobashiriwa Pepo: Abu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhiya Allaahu 'Anhu) - 2

 

 

Fadhila za Wahamaji (Muhajirina)

 

 

Kuna Aayah na Hadiyth nyingi zinazotaja fadhila za wahamaji (Muhajirina) Mmoja wao ni Abu Bakr ‘Abdullaah bin Abi Quhaafah Al-Taymy Kauli ya Allaah inasema,

“Wapewe mafakiri Wahajiri waliotolewa majumbani mwao na mali yao kwa ajili ya kutafuta fadhila kutoka kwa Allaah na radhi Zake, na wanamsaidia Allaah na Mtume Wake. Hao ndio wakweli.” (59: 8)

 

Na vile vile katika Kauli ya Allaah :

“Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume, basi Allaah Alikwishamnusuru walipomtoa waliokufuru, naye ni wa pili katika wawili walipo kuwa katika pango, naye akamwambia sahibu yake: Usihuzunike. Hakika Allaah Yu pamoja nasi. Allaah Akamteremshia utulivu Wake, na akamuunga mkono kwa majeshi msiyoyaona, na akalifanya neno la waliokufuru kuwa chini, na Neno la Allaah kuwa ndilo juu. Na Allaah ndiye Mwenye nguvu Mwenye hikima.” (9: 40)

 

‘Aaishah, Abu Sa’id na Ibn ‘Abbaas walisema; “Abu Bakr alikuwa pangoni na Mtume katika pango la Ath-Thawr, Makkah).” (Al-Bukhaariy).

 

 

Habari za Peponi Zinazofurahisha

 

 

Mtume asiyezungumza kwa utashi wake, alimletea Abu Bakr habari zinazofurahisha za Peponi zaidi ya mara moja.

 

Anas bin Malik alisimulia: Hakika, Mtume, Abu Bakr ‘Umar na ‘Uthmaan walipanda mlima Uhud wakati mlima ukitetema, na hapo Mjumbe wa Allaah alisema: “Kuwa madhubuti ewe Uhud. Kuna Mtume, mtu mwaminifu mmoja, na mashahidi wawili wamesimama juu yako.” (Al-Bukhaariy Hadiyth Na. 3675).

 

Bila shaka yeyote alikuwa anamkusudia Abu Bakr kwa kauli yake: “Mtu mwaminifu” Imeridhiwa kuwa waaminifu na wa kweli ni miongoni mwa wenye haki ya kuwemo Peponi kwa mujibu wa maandiko ya Qur-aan kama Mola Alivyosema:

“Na wenye kumtii Allaah na Mtume , hao wa pamoja na wale aliowaneemesha Allaah miongoni mwa Manabii, na Masiddiqi, na Mashahidi, na Watu wema. Na uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao! “ (4: 69).

 

Abu Hurayrah alisimulia kuwa Mjumbe wa Allaah alisema: “Yeyote atakayetoa aina mbili ya vitu kama sadaka katika njia ya Allaah, ataitwa kwenye lango la Peponi na ataambiwa: “Ewe mtumwa wa Allaah! Neema iko hapa’ Yeyote aliyekuwa miongoni waliokuwa wakisimamisha Swalah, ataitwa kwenye lango la Swalah. Abu Bakr As-Swiddiyq na yeyote aliyekuwa miongoni mwa walioshiriki katika Jihaad, ataitwa kwenye lango la Jihaad, na yeyote ambaye alikuwa miongoni mwa wafungaji, ataitwa kwenye lango la Ar-Rayyaan; yeyote aliyekuwa miongoni mwa waliokuwa wakitoa As-Swadaqah, ataitwa kwenye, lango la As-Swadaqah.” Abu Bakr alisema: “Waruhusu wazazi wangu watolewe muhanga kwa ajili yake, Ewe Mjumbe wa Allaah! Hatopata dhiki yule atakayeitwa kwenye milango hiyo. Je, yupo atakayeitwa kwenye milango yote hiyo?”Mtume alijibu, “Ndiyo, na nataraji utakuwa mmoja wao.”

 

 

Siku ya Kutawafu Mtume

 

 

Waislamu walipata majonzi makubwa siku alipofariki dunia Mtume ‘Umar bin Al-Khattwaab aliathirika sana kiasi cha kuchomoa upanga wake na kusema: “Iwapo nitamsikia yeyote akisema kuwa Mjumbe wa Allaah amefariki dunia, nitakata shingo yake.”

 

Mjumbe alitumwa kwa Abu Bakr Yule mtu alipomwona Abu Bakr, alilia. Abu Bakr alimwuliza: “Una jambo gani? Mtume amefariki dunia?” Yule mtu alisema: “’Umar bin Al-Khattwaab anasema: “Sitomsikia yeyote akisema Mjumbe wa Allaah amefariki dunia bila kutaka kukata shingo yake.”

 

Abu Bakr aliingia ndani ya nyumba ambapo Mtume alilazwa na kufunikwa nguo. Alimbusu na alitoka nje na kuwasomea Aayah ifuatayo:-

“Na Muhammad hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwishapita kabla yake Mitume. Je, akifa au akauwawa ndiyo mtageuka mrudi nyuma? Na atakayegeuka akarudi nyuma huyo hatamdhuru kitu Allaah. Na Allaah Atawalipa wanaomshukuru.” (3: 144)

 

Na Aayah:

“Ni nani itakayemfikia adhabu ya kumhizi, na itakayemshukia adhabu ya daima.” (39: 30).

Kisha akasema: “Yeyote aliyekuwa akimwabudu Muhammad afahamu kuwa Muhammad amefariki dunia. Na yeyote aliyekuwa anamwabudu Allaah, afahamu ya kuwa Allaah ni wa milele na hatokufa.” ‘Umar alisema, “WaLlaahi! Inakuwa kama sikuwahi kuzisoma Aayah hizi mpaka leo.”

 

 

Utume Wake

 

 

Mjumbe wa Allaah hakuwahi kumteua kati ya Maswahaba zake kuwa Khalifa. Lakini katika siku zake za mwisho, alisema kama ilivyoelezwa katika Hadiyth ifuatayo:

“Amri aliyopewa Abu Bakr kuwaswalisha watu.”

‘Aaishah alisema: “Kwa uhakika, Abu Bakr ana moyo laini na kila wakati hulia. “Mjumbe wa Allaah alisema: “Mwamuru Abu Bakr awaswalishe watu.” Alijibu, “Kwa hakika Abu Bakr ana moyo laini, na atakaposimama katika nafasi yako, watu hawatomsikia: Akaendelea kusema: “Muamuru Abu Bakr awaswalishe watu. Wewe ni sawa na mwanamke kwenye kisa cha Yuusuf.”

 

Kwa hiyo, mjumbe (aliyetumwa kuwasilisha amri ya Mjumbe wa Allaah kuwaongoza watu katika Swalah) alifika kwa Abu Bakr na kumfahamisha juu ya suala lile. Hivyo ‘Abu Bakr ndiye aliyewaswalisha watu wakati wa uhai wa Mtume.

 

Baadhi ya Wanachuoni wamehitimisha kuwa kuanzia wakati ule na tukio lile la Mjumbe wa Allaah alimpasisha Abu Bakr kuwa Khalifa, kwa kuwa kuwaswalisha watu ni jukumu la kwanza na muhimu kwa Khalifa.

 

Baada ya Mtume kufariki dunia Al-Answaar (Waungaji mkono watu wa Madiynah) walijumuika chini ya kivuli cha Banu Saa’idah na kusema: “Sa’d bin Ubaidah atapewa Ukhalifa.”

 

Al-Muhajirina (Waliohamia Madiynah kutoka Makkah) walipata habari za mkusanyiko wa kuchagua Khalifa, nao walikwenda kuhudhuria. Mmoja wa Answaar alitoa hutuba. ‘Umar bin Al-Khattwaab   alitaka kutoa hutuba, lakini Abu Bakr alimwashiria akae kimya, na alifanya hivyo. Abu Bakr alisimama na kuhutubia. Hakuzoza jambo juu ya mema ya Answaar.

 

Alisema:

“Mnafahamu ya kuwa Mjumbe wa Allaah alisema:

“Endapo watu wangechukua bonde maalumu, na Answaar wakachukua jengine. Ningechukua bonde la Answaar. Nilichosema kuhusiana nanyi ni maadili yenu mema. Lakini Waarabu hawakujua kadhia hii isipokuwa Ma-Quraysh kwa sababu wao ni bora kuliko Waarabu wengine kwa wema. Nimewachagua watu hawa wawili kwa ajili ya kiapo cha utii. Kwa hiyo kuleni kiapo cha utii.”

Aliushika mkono wa ‘Umar bin Al-Khatwab na Abu ‘Ubaydah bin Al-Jaraah

 

Abu Bakr alipomaliza hatuba yake, Answaar walipendekeza kuwa na Ma-amir wawili, mmoja kutoka ‘Answaar na mwingine kutoka Mahajirina.

 

‘Umar alisema: “Mnajua ya kuwa Mjumbe wa Allaah alimuamuru Abu Bakr awaswalishe watu? Wakasema, “Ndiyo, hapana shaka.” Kawaambia “Nani atapewa kipaumbele; mtu mwingine asiyekuwa yule aliyetangulizwa na Mtume ?  Wakajibu: “Hayupo: (hapana)”.

 

Abu Bakr alisimama na kumwambia ’Umar Nyoosha mikono yako ili tule kiapo cha kukukutii” Lakini ‘Umar alikataa, na mkono wa Abu Bakr ili kula kiapo cha kumtii. Usayd bin Hudayr na Bashir bin Sa’d alimpa ahadi ya utiifu Abu Bakr na watu wengine waliohudhuria walifanya hivyo pia. Kwa hiyo wote Answaar na Muhajirina walichukua ahadi ya kumtii Abu Bakr Siku iliyofuatia, watu walijumuika kwa ajili ya Swalah. Abu Bakr alipopanda juu ya mimbari, kila mtu alikula kiapo cha kumtii.

 

 

Khutbah Yake Baada ya Kiapo Cha Utiifu

 

 

Abu Bakr alipochaguliwa kuwa Khalifa, alipanda juu ya mimbari kutoa hotuba, na alipokuwa akifanya hivyo, alionyesha mwenendo mwema. Aliheshimiwa kama Swahaba mwenye cheo. Alionyesha heshima na kumcha Allaah.

 

Baada ya kumshukuru Allaah alisema:

“Enyi watu! Nimechaguliwa kuwa Khalifa, hata hivyo mimi sio bora kuliko nyie. Kwa hiyo, kama nikipatia katika hukumu, niungeni mkono; vinginevyo mna haki ya kunikosoa. Ukweli ni uaminifu, na kuongopa ni uasi. Wadhaifu miongoni mwenu watapata nguvu mpaka nitakapowapoka haki zao; ambao watu wenye nguvu miongoni mwenu ni dhaifu kwangu mpaka nitakapowapoka haki yao, Allaah akipenda. Msiache Jihaad (kupigana kwa ajili ya Allaah ). Hapana watu waliacha Jihaad bila kughadhibikiwa na Allaah Nitiini wakati namtii Allaah na Mjumbe Wake. Nikiwaasi, nami sina haki ya kutiiwa.”

 

Kisha aliwaamuru wasimame ili waswali kwa kusema: “Simameni kwa ajili ya Swalah, na Allaah Awanyeshee huruma zake.”

 

Abu Bakr alihofia sana majukumu makubwa aliyobeba kama Khalifa, Qays bin Abu Hazm alisema: Nilipokuwa nimekaa na Abu Bakr Khalifa wa Mjumbe wa Allaah mwezi mmoja baada ya kutawafu Mtume . Kuliadhiniwa na watu walijumuika. Ilikuwa mara ya kwanza kusomwa Adhaana. Abu Bakr alipanda kweye mimbari, na akamtukuza Allaah. Kisha akasema:

“Enyi watu natamani mtu mwingine angepewa haya madaraka. Kama mmenitaka nitawale kama alivyofanya Mtume wenu, itakuwa nje ya uwezo wangu kwa sababu yeye alikuwa amehifadhiwa, na muhimu Zaidi alikuwa akipokea wahyi.”

 

 

Vita Dhidi Ya Walioritadi

 

 

Baada ya kufariki dunia Mtume, makabila mengi ya Kiarabu katika sehemu nyingi waliritadi (walibadili imani) isipokuwa Kaskazini mwa Madiynah ambapo makabila yaliona jeshi la Usaamah walitanabahi kuwa kama Waislamu wasinge kuwa na nguvu wasingeweza kusonga mbele umbali ule dhidi ya jeshi kubwa kama Usaamah alivyofanya. Kwa Abu Bakr halikuwa na jambo la muhimu zaidi ya mantiki. Ulikuwa ni uamuzi wa Mtume, na kwa hiyo ilikuwa lazima uheshimiwe bila kujali matatizo au vikwazo. Maagizo yake yalikuwa “Nilitumaini mbele jeshi la Usaamah. Naapa kwa Allaah iwapo mbwa mwitu watanishambulia, sitosita kupeleka jeshi. Kwani sitobadilisha maamuzi yaliyofanywa na Mjumbe wa Allaah .

 

Wartadi walikuwa makundi mawili.

·         Kundi la kwanza liliritadi kwa hofu na waliwafuata Mitume wa uongo, kama vile Musaylimah, Tulayhah na kadhalika.

 

·         Kundi jengine halikuacha Uislamu na waliendelea kuamini ya kuwa: “Hapana apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah, na kuwa Muhammad ni mtumwa Wake na Mjumbe wake. Hata hivyo, walikataa kutoa Az-Zakaah. Mgogoro wa kundi hili ulipelekwa kusuluhishwa kwa Khalifa (Abu Bakr).

 

‘Umar bin Al-Khattwaab  alikuwa mmoja na Maswahaba walioitwa kusikiliza mgogoro.

Abu Bakr alipinga kwa nguvu zake zote, alisimama imara kama jabali.

Hakuogopa Lolote na wakati huo alitoa hutuba yake maarufu:

“WaLlaahi, kama waliniamini hatamu ya mnyama waliyokuwa wakimpa Mjumbe  wa Allaah , nitapigana mpaka waisalimishe,

‘Umar alimwambia:

“Unawapigaje ambapo Mtume alisema: “Nimeamrishwa (na Allaah) kuwapiga wale wanaopigana, mpaka waseme: La illaha illAllaah (hapana mwenye haki ya kuabudiwa ila Allaah ). Na yeyote aliyesema, ataokoa maisha yake na mali yake, kwa kutovunja shari’ah (haki na hali zitakazonifanya aadhibiwe kwa haki (bila uonevu), na hesabu yake itakuwa kwa Allaah ”

 

Abu Bakr alisema:

“WaLlaahi! Nitawapiga wale wanaotofautisha kati ya Swalah na Zakaah, kwa kuwa Zakaah ni haki ya lazima kuchukuliwa kutokana na mali (kwa mujibu wa Amri ya Allaah). WaLlaahi! Watakapokataa kunilipa hata ugwe waliokuwa wakitoa zama za Mjumbe wa Allaah, nitawapiga mpaka watoe walichozuia.”

    

Maswahaba wa Mtume walikuwa na rai kuwa Abu Bakr aamiliane na makafiri kwa upole, ‘Umar alikuwa mmoja wao. Alimwambia:

“Ewe Khalifa wa Mjumbe wa Allaah !  Kuna mpole na mwenye huruma kwa watu.”

 

Abu Bakr alikasirika na kumwambia:

“Nilitarajia msaada wako, lakini umeniacha mkono. Je, inafaa kuwa wakorofi katika siku za ujahili na dhaifu katika Uislamu? Wahyi umesimama, na sasa Dini imekamilika. Inahoofika wakati bado niko hai! Kama Mjumbe wa Allaah asingesema: Isipokuwa lile lililofaradhishwa.’ Kwa hali hiyo, tutasimamisha Swalah, na kuwalipa masikini haki yao. WaLlaahi, hata kama watu wote wasinisaidie, nitapigana nao peke yangu.” Wasaidizi wa waasi (murtadi) waliona uchache wa askari wa Kiislamu, Madiynah baada ya kutoka kwa jeshi la Usaamah. Hali hii iliwafanya washambulie.

 

Abu Bakr alikuwa amechukua tahadhari, hivyo aliwatuma baadhi ya Maswahaba kwa makabila yaliyokuwa jirani ambao wangeshambulia Madiynah, na makabila hayo yalipigwa.

 

Abu Bakr aliongeza jeshi lililokuwa na Answaar na Muhajirina mpaka alipofika Naq (kauli ya Najd). Wakazi wa jangwani walikimbia pamoja na watoto wao. Watu walimtaka Abu Bakr arejee Madiynah na ateue kamanda mpya wa jeshi. Alimteua Khalid bin Al-Waliyd na akamwambia:

         

“Watu watakaporejea kwenye Uislamu na wakalipa haki za masikini, iwapo mmoja wenu anataka kurejea na arejee.”

         

Abu Bakr alirejea Madiynah wakati jeshi la Usaamah lilikuwa limepata ushindi. Jeshi la Usaamah lilipopumzika, Abu Bakr alikusanya vikosi kumi na moja chini ya Khaalid bin Al-Waliyd, ‘Ikrimah bin Abu Jahl., ‘Amr bin Al-‘As, Sawayd bin Maqrin, Al-‘Ala Bin al-Haddramiy na wengineo.

 

 

Vita Vya Buzaakhah

         

Vita vya Buzaakhah vilikuwa vita maarufu dhidi ya makafiri. Abu Bakr alimuelekeza Khalid bin Al-Waliyd kupigana dhidi ya Mtume mwingine na bandia aliyeitwa Tulayhah bin Khuwaylid Al-Asadi.

         

Abu Bakr alimwamuru ‘Adiy bin Haatim aende Tay (kabla ya kumwamuru Khaalid bin Al-Waliyd Alimwamuru ‘Adiy aanzie Tay, kisha aelekee Buzaakhah na kisha Al-Batah. Aliambiwa hata kama alipata ushindi, hakutakiwa kuondoka mpaka apewe rukhsa na Abu Bakr Ki-istratejia, Abu Bakr alisema watoke na jeshi wakakabiliane na jeshi pinzani lililoongozwa na Khaalid bin Al-Waliyd kama njia ya kuwahofisha.

 

 

Vita Ya Al-Yamaamah

 

Al-Yamaamah ilikuwa nchi ya asili ya Banu Haniyfah iliyopo katikati ya Rasi ya Arabia, Kaskazini ya Najraan. Lilikuwa eneo lenye mimea mingi na mitende mingi na hapo ndipo Khaalid bin Al-Waliyd alipigana dhidi ya Musaylimah, mzandiki mkubwa. Musaylimah alikuwa miongoni mwa wasaidizi wa Banu Haniyfah ambao walikwenda kwa Mjumbe wa Allaah (mwaka wa makaimu). Aliporejea, alijidai kuwa mwenza wa Mjumbe na akawaongeza watu wake kwenye bid’ah na kuwaweka mbali na Uislamu.

         

Baada ya kifo cha Mtume , Abu Bakr alimtuma ‘Ikrimah bin Abi Jahl na kisha akamtuma Shurahbiyl bin Hasanah kupigana na Musaylimah, lakini Ikrimah alishindwa. Abu Bakr alimuelekeza Shurahbiyl kwa watu wa Oman, na alimwamuru akae mpaka Khaalid atakapoungana naye wampige Musaylimah kwa pamoja.

         

Jeshi la Waislamu lilipokabiliana na jeshi la Musaylimah, Zayd bin Al-Khattwaab alikuwa upande wa kulia kwa Khaalid na Abu Hadhayfah bin ‘Utbah alikuwa upande wa kushoto. Bendera la Answaar lilibebwa na Thaabit bin Qays bin Shammar bendera la Muhajirina lilibebwa na Saalim (mtumwa aliyeachwa huru na Abu Hadhayfah) Wafuasi wa Musaylimah walikuwa elfu kumi ambao walipigana kwa nguvu.   

 

Waislamu walipigana mpaka wakakaribia kushindwa. Baadhi ya Waislamu walihisi hatari ya kushindwa kutokana na ukubwa wa jeshi la adui, kwa hiyo wakapeana moyo kuwa imara katika mapambano. Thaabit bin Qays alisema:

“Ee Allaah! Nakanusha yale wayafanyayo (yaani watu wa Al-Yamaamah) na nakuomba msamaha kwa yote wayafanyayo (yaani Waislamu).

Kisha alimshambulia adui na kumuua. Zayd bin Al-Khattwaab alisema:

“WaLlaahi, sitozungumza tena mpaka nimshinde.” Vita iliendelea kuwa kali na Saalim, Abu Hudhayfah na Zayd bin Al-Khattwaab waliuawa.

 

Khaalid bin Al-Waliyd alitanabahi ya kuwa kusingekuwa na ushindi wa uhakika mpaka wamwue Musaylimah. Kwa hiyo alishambulia huku akipiga ukulele… Kila mtu aliyejitokeza aliuawa. Musaylimah na aliokuwa nao baada ya kuona hali ile walikimbilia bustanini. Al-Bara’ bin Maalik alisema:

“Enyi Waislamu! Nitupeni ndani ya bustani. Waislamu walisita kwa kumwogopa, lakini walifuata amri yake, na alitupwa ndani ya bustani mpaka akapigana vita kali Musaylimah aliuawa. ‘Wahshi (mtumwa aliyeachwa huru na Jubayr, aliyemuua Hamzah  ‘ami yake Mtume, siku ya Uhud) alimuua Musaylimah waliuawa kwa sababu jeshi la Waislamu lilikuwa imara. Allaah Aliwasaidia mpaka wakamshinda adui.

 

 

Ukusanyaji Wa Qur-aan Tukufu Kuwa Mus-haf Mmoja

         

Matokeo ya vita vilivyopiganwa kati makafiri na Waislamu, Maswahaba maarufu wa Mtume waliuawa. Miongoni mwao ni wale waaminifu waliohifadhi Qur-aan Takatifu. ‘Umar alichelea kuwa maandishi ya Qur-aan yangepotea kama vifo hivyo vingeendelea, na alimtaka Abu Bakr atoe amri ya kukusanywa kwa Qur-aan Tukufu ambako kutafanywa mara moja. Abu Bakr hakupenda kufanya jambo ambalo Mtume hakulifanya mwenyewe, lakini alijua ya kuwa ‘Umar alikuwa sahihi, vinginevyo Qur-aan ingeweza kupotea baada ya muda. Abu Bakr alikubaliana na fikra za ‘Umar hivyo alimuamuru Zayd bin Thaabit akusanye matini ya Qur-aan.

 

Alisimulia Zayd bin Thaabit (mwandishi wa Qur-aan Tukufu). “Abu Bakr As-Swiddiyq aliniita wakati watu wa Yamaamah walipouawa (yaani Maswahaba wengi wa Mtume waliopigana na Musaylimah). Nilikwenda kwake na nilimkuta ‘Umar bin Al-Khattwaab amekaa naye. Abu Bakr aliniambia, “‘Umar alikuja kwangu na kuniambia:

“Qur-aan wengi walifariki dunia (yaani waliohifadhi Qur-aan) siku ya vita ya Yamaamah na nachelea wengi wao wanaweza kuwa mashahidi katika vita vingine na sehemu kubwa ya Qur-aan hupotea. Kwa hiyo, nakushauri wewe (Abu Bakr) utoe amri Qur-aan ikusanywe.” Nilimwambia ‘Umar: ‘Unawezaje kufanya jambo ambalo Mjumbe wa Allaah hakulifanya?”  ‘Umar alijibu: ‘WaLlaahi, hili jambo zuri la kufanywa, “‘Umar aliendelea kunishawishi nikubali pendekezo lake mpaka Allaah Alipofungua kifua changu na kuanza kuona uzuri wa rai ya ‘Umar. “Kisha Abu Bakr aliniambia, “Wewe ni kijana mwerevu, na hatuna shaka nawe. Ulikuwa ukiandika Ufunuo Mtakatifu kwa kuongezwa na Mjumbe wa Allaah kwa hiyo tafuta maandiko ya Qur-aan na yakusanye yawe kitabu kimoja.”

 

WaLlaahi! Kama wangeniamuru kuhamisha moja ya milima, isingekuwa mizito katika ombi hili. Kisha nilimwambia Abu Bakr,” Utafanyaje jambo ambalo Mtume hakulifanya?” Abu Bakr  aliendelea kunishawishi nikubaliane na rai yake mpaka Allaah Alipofunua kifua changu kwa kile alichofunua kifua cha Abu Bakr na ‘Umar  Kwa hiyo nilianza kuitafuta Qur-aan na kuikusanya kutokana (na yale yaliyoandikiwa juu yake) makuti ya mtende, mawe meupe membamba na kutoka kwa watu waliojua kwa moyo, mpaka nilipoipata ayah ya mwisho ya Surat Al-Tawbah kwa Abi Khuzaimah Al-Answaari, na Aya hiyo niliikuta kwake tu. Aya yenyewe ni hii:

“Hakika amekwishakujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma.

Basi wakigeuka, wewe sema: Allaah Ananitosheleza. Hapana mungu isipokuwa Yeye tu. Mimi namtegemea Yeye, na Yeye ndiye Mola Mlezi wa Kiti Kikuu cha Enzi.” (9: 128,129).

 

Muswada kamili na Qur-aan ulibaki kwa Abu Bakr mpaka alipofariki dunia, kisha akawa kwa ‘Umar mpaka alipofariki dunia, kisha kwa Hafswah, binti ya ‘Umar. (Al-Bukhaariy, Hadiyth Na. 4986).

 

Ilisimuliwa kwa mamlaka ya ‘Aliy:

“Malipo bora juu ya (ukusanyaji wa) Mushaf yamwendee Abu Bakr Alikuwa na mwanzo kurekodi Qur-aan Tukufu.”

 

 

Hadhi  Yake

 

Hapana shaka kuwa Abu Bakr alikuwa na hadhi ya kipekee miongoni mwa Maswahaba wa Mjumbe Kuna Hadiyth nyingi zinazothibitisha ya kuwa alikuwa anapendwa Zaidi na Mtume Kuna Hadiyth nyingi zinazothibitisha ya kuwa alikuwa anapendwa Zaidi na Mtume na alikuwa rafiki yake kabla na baada ya kutangaza Uislamu. Mtume hatosahau kuwa alikuwa wa mwanzo kusilimu. Maswahaba walijua hadhi yake kwa Mtume na walijua alivyotumia kwa ajili ya Dini. Ni kwa sababu hii walimheshimu sana na wakaweka hadhi yake kwenye ndimi na mioyo yao. Wakati wote alikumbukwa na kusemwa kwa heshima na uchaji wake. Alimpenda kwa sababu mbili. Ya kwanza, kwa sababu ya tabia yake kama vile ukarimu, wema, ukweli, msafi (asiye na dhambi kubwa) na kuwa wa kwanza katika Uislamu na ya pili mapenzi kwa Mtume

 

Amr bin Al-‘Aas alisema:

“Mtume alinitumia kamanda wa jeshi aliyeitwa Dhatus–Salaasil. Nilimwuliza: “Nani unayempenda zaidi? Akajibu, ‘Aaishah. Nikamwambia, ‘Katika wanaume’ Akajibu “Baba Yake.” Kisha nikasema: ‘Kisha nani? Akajibu: ‘‘Umar bin Al-Khattwaab . Kisha Mtume aliwataja wanaume wengine.”

           

Mtume katika Hadiyth nyingi anawafafanulia Maswahaba sababu ya kumpenda zaidi Abu Bakr. Msikilize asemavyo.

“Kwa uhakika Allaah alinituma kwenu. Mkaniambia: ‘Unasema uongo’, ambapo Abu Bakr (aliniamini na) akawambia watu, ‘Anasema kweli, na akanifariji.” Kisha alisema mara mbili, “Basi hamuachi kumdhuru mwenzangu?” Baada ya pale hapana aliye mdhuru Abu Bakr. (Al-Bukhaariy 2661.)

         

Shukrani za Mtume zinaweza kuonekana katika kauli yake:

“Abu Bakr amenipendelea kwa mali yake na usuhuba wake. Kama ningetakiwa kuwa na Khaliyl miongoni mwa binaadamu, bila shaka ningemchukua Abu Bakr lakini udugu wa Kiislamu na urafiki unatosha. Fungeni milango yote ya Msikiti isipokuwa ule wa Abu Bakr.” (Al Bukhaariy 3654.)

         

Kwa mamlaka ya ‘Abdullaah bin Shaqiyq ambaye alisema ya kuwa alimwambia ‘Aaishah:

“Nani kati ya Maswahaba wa Mjumbe wa Allaah alipendwa sana naye?” Alijibu, “Abu Bakr” Nilisema, “Kisha nani?” Alijibu “‘Umar” Nikasema “Kisha nani?” Alijibu, “Abu ‘Ubaydah” nilimwambia kisha nani?” Alinyamaza kimya. (Sunan At-Tirmidhiy 3657.)

 

Daraja ya Abu Bakr ilikuwa ya juu baada ya Mitume (kwa ubora).

“Alisimulia Ibn ‘Umar. Tulikuwa tukiwalinganisha watu kuona ni yupi bora wakati wa uhai wa Mjumbe wa Allaah Tulimwona Abu Bakr kuwa bora zaidi, kisha ‘Umar na kisha ‘Uthmaan ”

         

Inafahamika ya kuwa Mtume alipenda na kuchukia kwa ajili ya Allaah. Kwa hiyo mfahamu ya kuwa hadhi ya Abu Bakr ilipokuwa ya juu mbele ya Allaah kwa kuwa ilikuwa juu kwa Mtume

 

Mjumbe wa Allaah alisema:

“Kwa hakika watu wenye daraja la chini watawaona wale wenye daraja la juu kama muonavyo nyota zing’arazo upeo wa macho. Na kwa hakika, Abu Bakr na ‘Umar ni miongoni mwa hao.”

 

 

Imani  Naye

 

Kutokana na kuwa karibu na Mtume tunaona tabia ya Abu Bakr ilikuwa uaminifu wake, ukweli na kupenda haki. Alitegemewa kwa masuala ya sekula na Dini na aliamuru Abu Bakr aongoze Swalah alipokuwa mgonjwa sana. Watu wote walichukulia tukio hilo kuwa Abu Bakr atakuwa Khalifa, kwa kuwa kuswalisha watu ni jukumu la Khalifa. Hili linathibitishwa na maneno ya Mtume:

“Sijui nitakuwa nanyi kwa muda gani, kwa hiyo fuateni mwongozo wa watu wawili watakaochukua uongozi baada yangu”, na akamnyooshea kidole Abu Bakr na ‘Umar.” (At- Tirmidhiy 3664.)

         

Hivi Mjumbe wa Allaah anawaamuru watu wafuate uongozi wa mtu yeyote isipokuwa yule mwenye kuaminika.

         

‘Aaishah amesema kuwa Mtume alisema,

“Hainipitikii akilini ya kuwa mtu mwingine angekuwa Imaam katika Swalah, wakati Abu Bakr alikuwa miongoni mwao.”

 

Ibn ‘Abbaas alisimulia ya kuwa Mtume alisema:

“Kama ningetakiwa kuwa na Khalili, ningemchukua Abu Bakr, lakini yeye ni ndugu yangu na mwenzangu (katika Uislamu)” (Al-Bukhaariy).

 

Na Ayyuub alisimulia ya kuwa Mtume alisema,

“Kama ningetakiwa kumchagua Khalili, ningemchukua yeye (yaani Abu Bakr) kuwa Khalili, lakini udugu wa Kiislamu ni bora.” (Al-Bukhaariy).

 

Kuna Hadiyth nyingine inayothibitisha uaminifu huu. Jubayr bin Mut’im alisimulia.

         

Mwanamke alifika kwa Mjumbe wa Allaah na kuzungumza naye. Alimtaka aseme hoja yake, na alisema; “Nitafanya nini. Ewe Mjumbe na Allaah, nitakapokuja nikakukosa?” (kama alikuwa na maana, “Nikikuta umefariki dunia) Alimjibu “Usiponikuta, nenda kwa Abu Bakr.” (Al-Bukhaariy Hadiyth Na. 3659)

 

 

Uaminifu huu wa Mjumbe wa Allaah ulipenya nyoyo za Waislamu. Kutokana na hali hiyo watu wengi walikuta kigogo cha utii na akapata uungwaji mkono, na maazimio ambayo yaliathiri kwa kiasi kikubwa kukua kwa dola ya Kiislamu.

 

 

Share