Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Tafsiyr Gani Anatakiwa Awe Nayo Mtafutaji Elimu?

 

 Tafsiyr Gani Anatakiwa Awe Nayo Mtafutaji Elimu?

 

Imaam Muhammad bin Swaalih Al-‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Allaah Awahifadhi na Azinyooshe hatua zenu, Twaalib Al-‘Ilm (Mwanafunzi, Mtafutaji elimu) anataka kusoma Tafsiyr, ni zipi Tafsiyr mashuhuri ambazo anahitaji kuwa nazo mwanafunzi?

 

 

JIBU:

 

 

Maona amiliki Tafsiyr ya Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah), na Tafsiyr ya Shaykh wetu ‘Abdur-Rahmaan As-Sa’diy, kwani hizo mbili ni Tafsiyr bora nilizozipitia katika vitabu vya Tafsiyr.

Vilevile kuna Tafsiyr zingine kwa mtafutaji elimu mwenye shauku na kutaka (kusoma), kama vile Tafsiyr ya Al-Qurtwubiy na Tafsiyr Ash-Shawkaaniy. Na’am.

 

 

[Al-Mawqi’ Ar-Rasmiy li-Fadhwiylah Ash-Shaykh Al-'Allaamah Muhammad bin Swaalih Al-'Uthaymiyn]

 

 

N.B. Katika sehemu nyingine, Imaam Ibn ‘Uthaymiyn vilevile aliitaja Tafsiyr ya Ibn Jariyr Atw-Twabariy kuwa ni katika Tafsiyr bora ila inahitaji mwenye maarifa kutokana na upana wa ufafanuzi wake na wingi wa maelezo ya wapokezi wa Ahaadiyth, Athaar na Isnaad.

 

 

Share