02-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Posa Na Hukumu Zake: Ni Nani Anayekabidhiwa Posa?

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

الخِطْبَةُ وأَحْكَامُهَا

 

Posa Na Hukumu Zake

 

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

02:  Ni Nani Anayekabidhiwa Posa? 

 

1-  Kiasili, posa inapelekwa kwa walii wa mwanamke:

 

Toka kwa ‘Urwah:

 

"أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ خَطَبَ عَائِشَةَ إِلَى أَبِي بَكْرٍ، فَقَالَ لَهُ أَبُو بَكْرٍ: إِنَّمَا أَنَا أَخُوكَ، فَقَالَ: ‏أَنْتَ أَخِي فِي دِينِ اللَّهِ وَكِتَابِهِ وَهِىَ لِي حَلاَلٌ"

“Kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimweleza Abu Bakr shauri la kumposa ‘Aaishah.  Abu Bakr akamwambia:  “Hakika mimi ni nduguyo.  Rasuli akamwambia:  “Wewe ni ndugu yangu katika Dini ya Allaah na Kitabu Chake, lakini yeye kwangu ni halali”.  [Imechakatwa na Al-Bukhaariy (5081)]

 

2-  Mwanamke mkomavu anayejitambua anaweza kupokea posa ya kuchumbiwa yeye mwenyewe au kuikataa:

 

Ni kwa Hadiyth ya Ummu Salamah:

 

"لَمَّا مَاتَ أَبُو سَلَمَةَ أَرْسَلَ إِلَىَّ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ‏حَاطِبَ بْنَ أَبِي بَلْتَعَةَ يَخْطُبُنِي لَهُ فَقُلْتُ: إِنَّ لِي بِنْتًا وَأَنَا غَيُورٌ‏"‏ ‏

 

“Alipokufa Abu Salamah, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimtuma Haatwib bin Abu Balta’ah aniletee posa yake ya kunichumbia mimi.  Nikamwambia:  Mimi nina binti, na mimi nina wivu sana”.  [Hadiyth Swahiyh.  Muslim na An-Nasaaiy (6/81)]

 

 

 

Share